Ask. Ngalalekumtwa awataka waamini kumuombea Rais Magufuli


Na Getrude Madembwe, Iringa.

ASKOFU Tarcisius Ngalalekumtwa wa Jimbo Katoliki Iringa amewataka waamini kumuombea Rais Dk. John Magufuli na serikali yake ili aweze kuliongoza Taifa kwa haki na amani.


Askofu Ngalalekumtwa ambaye pia ni Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) ameyasema hayo hivi karibuni wakati wa Misa Takatifu ya Pasaka katika Kanisa Kuu la Moyo Mt. wa Yesu Parokia ya Kihesa Iringa.

“Amani tuliyonayo ni tunu kutoka kwa Mungu hivyo watanzania tunapasika kuilinda, tumuombee pia Rais wetu na serikali yake ili iwe yenye huruma na inayoongoza kwa kufuata msingi ya haki .
 Pasaka hii inatufundisha kutendeana mema, Tunapoadhimisha pasaka kila mmoja wetu atafute haki, amani, atambue na aone kuwa mwenzake anastahili kulindwa na kutendewa haki.
Wadogo na wanyonge wapewe upendeleo katika akili zao na ndipo Mungu wetu atapendezwa maana ametoa jukumu kwa kila mmoja wetu kuwalinda na kuwajali wanyonge na wenye shida,” amesema Askofu Ngalalekumtwa.

Amewataka waamini kuombea ustawi wa imani yao na hasa kwa kipindi hiki wanapomshukuru Mungu kwa miaka 150 ya uinjilishaji .


“Haitoshi mtu kujiita mkristo kwa maneno, tuishi Injili kwa matendo tukikumbatiwa na unyenyekevu ndani ya moyo, upole, utulivu na amani ili kuleta tumaini jipya na wokovu katika jamii,” amesisitiza Askofu Ngalalekumtwa.

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU