DC Geita aunga mkono matamko la maaskofu

Na Marco Kanani, Geita
Mkuu wa Wilaya ya Geita Herman Kapufi amesema anaunga mkono Waraka wa Maaskofu wa Kanisa Katoliki katika kipindi cha Kwaresima akisema kuwa, una sauti ya kinabii.
Amesema hayo wakati akitoa salamu Misa Takatifu ya Mkesha wa Pasaka jimboni Geita amabyo iliongozwa na Askofu wa Jimbo Katoliki Geita Mhashamu Flavian Kassala.

“Binafsi amaejitahidi kuusoma kwa makini waraka huo wa Maaskofu na sikuona chochote kibaya katika waraka huo kwani yote yaliyomo ni mema sana.

Mimi niseme tu kuwa, mti wowote ambao ni mgumu kama hautaki kupinda wenyewe ukilazimishwa ama kupindishwa na upepo hautabaki salama lazima utavunjika hivyo sisi kama serikali tuko tayari kujirekebisha pale ambapo tunakosea, "amesema DC Kapufi.

Amesema, anachojua yeye ni kuwa kabla ya Maaskofu hawajaandika waraka wanasali kwanza na kumshirikisha Mungu mawazo yao, hivyo wakitoa neno linakuwa na upako wa kimungu na hivyo nyaraka zao zimejaa maono matakatifu.

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU