UJUMBE WA PAPA FRANSISKO KWA SIKU YA 26 YA WAGONJWA DUNIANI 2018


“TAZAMA huyo ndiye mwanao … tazama huyo ndiye mama yako. Na tangu saa ile huyo mwanafunzi alimchukua akae nyumbani kwake”(Yoh. 19:26-27), ni utangulizi wa Ujumbe wa Papa Fransisko kwa siku ya 26 ya Wagonjwa Duniani hapo mwaka 2018, ambapo amesema kuwa Kanisa na wahudumu wa wagonjwa wanapaswa kufanya huduma zao kwa uaminifu wa utume wa Bwana. (Lk 9,2-6: Mt 10,1-8; Mk 6,7-13).
Kauli mbiu ya Siku ya Wagonjwa Duniani 2018 imechaguliwa kutoka katika  maneno ya Yesu aliyotamka msalabani, akimwelekea mama yake Maria na Yohane: Mama wa Kanisa “Tazama huyo ndiye mwanao … tazama huyo ndiye mama yako. Na tangu saa ile huyo mwanafunzi alimchukua akae nyumbani kwake” (Yh 19:26-27). 
Katika ujumbe huo, Baba Mtakatifu anasema, Maneno ya Kristo yanaangaza kwa kina fumbo la Msalaba. Maneno hayo hayawakilishi janga hilo bila matumaini, bali ni mahali ambapo Yesu anaonesha utukufu wake alijiachia kwa utashi wa upendo wake upeo.
Amesema kuwa maneno ya Yesu yanatoa chanzo cha wito wa umama wa Maria mbele ya binadamu wote. Yeye kwa namna ya pekee anakuwa mama wa mitume na mwanae. Anachukuwa wajibu wa kuwatunza na katika safari yao. Wote tunatambua kuwa utunzaji wa mama kwa mwanae huanzia katika mantiki zote ziwe katika nyenzo na hata kiroho kwa mafundisho yake.
Injili inasema, “katika uchungu ulio kama upanga mkali utauchoma moyo wa Maria” (Lk2,35) lakini haumwogopeshi. Badala yake, kama Mama wa Bwana anaanza yeye safari moja kwa moja ya kujitoa yeye binafsi. Akiwa msalabani, Yesu anahangaikia Kanisa na binadamu wote, na Maria anaitwa kushirikishwa wasiwasi wa Yesu.
Baba Mtakatifu Fransisko anasema kuwa, katika kitabu cha Matendo ya Mitume, kikielezea juu ya tukio la Roho Mtakatifu Siku ya Pentekoste, kinaonesha kuwa Maria alianza shughuli yake katika Jumuiya ya kwanza ya Kanisa. Ni kazi ambayo haina mwisho.
Mtume Yohane, mpendwa, anawakilisha Kanisa, ambao ni watu kinabii. Yeye ni lazima atuambie kuwa Maria  ni mama yake. Na katika utambuzi huo, anaalikwa kupokea na kutafakri Maria  kama mfano wa utume na hata wito wa mama ambaye Yesu amemkabidhi, ikiwa ni pamoja na wasiwasi wake na mipango yote itokanayo na wito huo; kwa maana  ni mama anaye penda na kuzaa watoto wenye uwezo wa kupenda kwa mujibu wa amri ya Yesu.
Kwa njia hiyo wito wa mama Maria yaani wito wa kutunza watoto wake, unapitia kwa njia ya Yohane na Kanisa zima. Na Jumuiya nzima ya mitume wanahusika katika wito wa mama Maria.
Yohane kama mtu anayeshirikishwa na Yesu kila kitu anatambua jinsi gani Mwalimu wake anataka kuwakusanya watu wote wakutane  na Baba.Yeye anaweza kushuhudia kuwa Yesu alikutana na watu wengi wakiwa wagonjwa wa kiroho  na kwa sababu wamejaa kiburi (Yh 8,31-39) pia wagonjwa kimwili (Yh 5,6). Na kwa watu wote aliwapa huruma na msamaha.
Na wagonjwa kimwili wakapona, na ishara ya maisha yaliyojaa Ufalme, ni mahali ambapo machozi yanakaushwa. Kwa njia hiyo, kama Maria, mitume wanaalikwa kuhudumiana. Pia wanatambua ya kwamba, moyo wa Yesu huko wazi kwa wote bila ubaguzi. Wote wanapaswa kupashwa habari ya Injili ya Ufalme, wote ambao wanahitaji, wanapaswa kuelekezwa katika upendo wa kikristo kwa urahisi, kwa sababu ni watu, na wana wa Mungu.
Wito wa umama katika Kanisa, kwa ajili ya wahitaji na wagonjwa umejidhihirisha katika historia ya miaka elfu mbili iliyopita, katika utajiri wa kuanzisha mipango mingi kwa ajili ya wagonjwa. Ni historia ya kujikita katika shughuli hiyo bila kusahau.
Hata leo hii inaendelea katika dunia. Baba Mtakatifu anafafanua kuwa, katika nchi ambazo kuna mipango ya Afya ya umma inayojitosheleza, shughuli ya mashirika Katoliki, katika majimbo na mahospitali, zaidi ya kutoa tiba za hali ya juu pia wanatafuta kwanza kumweka  binadamu awe ni kitovu katika mchakato wa tiba na kuendelea na utafiti wa kisayansi kulingana na maisha na thamani zake za kimaadili ya kikristo.
Katika nchi ambazo kuna uhaba wa mipango ya afya, au kutokuwapo kabisa, Kanisa linajikita kutoa kile ambacho inawezekana kwa watu, kama vile utunzaji na afya, ili kuondoa na kupunguza vifo vya watoto wachanga. Aidha hata kuwasaidia baadhi ya wengine wenye magojwa ya kuambukiza.
Kila mahali Kanisa linajitahidi kutibu, hata kama halina uwezo wa kuponyesha. Sura ya Kanisa “kama hospitali iliyoko katika kambi”, inapokea wote waliojeruhiwa katika maisha. Ni hali halisi na ya dhati kwa sababu katika maeneo mengi ya ulimwengu, zipo hospitali za wamisionari na katika majimbo ambayo wanatoa huduma ya tiba muhimu kwa watu.
Kumbukumbu ndefu ya kihistoria ya huduma kwa wagonjwa; ni sababu ya furaha kwa jumuiya ya kikristo na kwa namna ya pekee kwa wale wanaotoa huduma hiyo nyakati za sasa. Baba Mtakatifu anafafanua kuwa ili kuweza kufanya hivyo, ni lazima kutazama yaliyopita ili kujitajirisha kutokana nayo.
Yote hayo ni lazima kujifunza kutokana na ukarimu hadi kujitoa sadaka ya moja kwa moja kwa waanzilishi wengi wa mashirika ya huduma ya wagonjwa kama vile ubunifu unaoelekezwa kutokana na upendo, shughuli nyingi zilizoanzishwa katika miongo mingi, shughuli za utafiti kisayansi, ili kuweza kutoa tiba kwa wangojwa kwa njia ya ubunifu na matibabu ya kuaminika. 
Anathibitisha zaidi kwamba, urithi huo wa kizamani unasaidia kupanga vizuri mipango ya baadaye.
Kwa Maria, Mama wa huruma, tunataka kumtolea wagonjwa wote, ikiwa ni kimwili na kiroho, ili awaweke katika tumaini. Kwake yeye tunamwomba pia kutusaidia tuwe wakarimu kwa kuwapokea ndugu wagonjwa. Kanisa linatambua kuwa na haja ya neema malumu ili kuweza kujikita katika huduma yake kiinjili kwa ajili ya wagonjwa. Kwa njia ya sala kwa mama wa Bwana, atutazame wote tunaounganika katika maombi ili kila mwanachama wa Kanisa awe hai na upendo wa wito wa huduma ya maisha na Afya.
Baba Mtakatifu anamalizia ujumbe wake akisema, Bikira Maria aombee siku ya 26 ya Wagonjwa duniani, asaidie wagonjwa wote waishi katika mateso yao na muungano na Bwana Yesu; awasaidie hata ambao wanawasaidia katika matibabu. Na kwa wote: wagonjwa, wahudumu wa Afya, watu wa kujitolea, anawapa Baraka yake.
Vatikani Novemba 26, 2017
Sikukuu ya Bwana wetu Kristo Mfalme wa Ulimwengu

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU