2124 kuhitimu SAUT

Na George Alexander, Mwanza

WAKATI Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino Tanzania (SAUT) Mwanza kikijiandaa na mahafali ya 19 yatakayofanyika Desemba 8 na 9, 2017, takribani wanafunzi 2124 sawa na asilimia 79 wanatarajia kuhitimu masomo yao huku wanafunzi 424 wakishindwa kuhitimu elimu yao ya chuo kutokana na sababu mbalimbali.
Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari chuoni hapo Makamu Mkuu wa SAUT Padri Dkt. Thaddeus Mkamwa amebainisha kuwa takribani wanafunzi 424 sawa na asilimia 21 ya jumla ya idadi ya watakaohitimu mwaka huu watashindwa kupata vyeti vyao vya ngazi ya cheti stashahada na shahada
Padri Mkamwa amebainisha kuwa wanafunzi wengi wameshindwa kuhitimu kwa sababu ya uzembe wa kitaaluma, wengine kushindwa kulipia gharama za masomo na pia baadhi matatizo ya kiafya
Kuhusu wanafunzi walioshindwa kuhitimu kwa sababu ya kitaaluma, Padri Mkamwa amesema kuwa wengi wao walishindwa katika masomo yao na wengine kushindwa kumaliza masomo yao ya utafiti ambayo kama mwanafunzi wa SAUT hutakiwa kufanya utafiti.
Pia maandalizi hayo ya mahafali hutanguliwa na siku ya kijamii ya SAUT ambapo wanafunzi na wahadhiri wao huitumia kwa ajili ya maonesho ya kitaaluma ambapo pia Makamu Mkuu wa chuo amewaomba wanafunzi ambao wameshindwa kudahiliwa chuoni hapo na pia kushindwa kupata pesa zao za mkopo, chuo kimezungungumza na benki ya CRDB na kukubaliana nao na wanafunzi wanatakiwa kuwasiliana na binki hiyo kwa utaratibu waliojiwekea
Mahafali ya 19 ya SAUT yatafanyika katika viwanja vya Rila Odinga na yataanza na adhimisho la misa takatifu ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Mwanza Mhashamu Yuda Thaddeus Ruwa’ichi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya wamiliki wa Vyuo, huku Mkuu wa Chuo hicho atawakilishwa na Askofu wa Jimbo Katoliki Geita Mhashamu Flavian Kasalla na Askofu wa Jimbo Katoliki Mbinga Mhashamu John Ndimbo. 


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU