Watawa waonywa dhidi ya matumizi ya mitandao

Na Dominic Maro
Mama Mkuu wa Shirika la Masista wa Mama Yetu wa Usambara COLU Sista Gaspara Kashamba awataka watawa wakijiepusha na vitu ambavyo vitavuruga utume wao ikiwepo simu ya mkononi kwani itawapotosha.
Amesema hayo kwenye Misa Takatifuikiwa ya kusherekea jubilei ya miaka 50, 25 na kuweka nadhiri za daima kwa Masista wa Shirika la Mama Yetu wa Usambara (Colu) Kwamndolwa, Korogwe Jimbo Katoliki Tanga
 “Umoja ndiyo msigi wa maisha ya utawa na kuyafuata yale yashirika ndiyo dira ya kutimiza utume wetu na chamuhimu katika maisha haya ni kujiepusha na yale ambayo yanawachanganya au kuwafuruga hasa matumizi ya mitanda ikiwemo simu ya mkononi kwani imeshawapoteza wengi hivyo masista wangu mjiepushe na hayo,” amesema sista Gaspara
Pia Sista Gaspara ametoa wito kwa mapadri wote nchini kutambua kuwa kila sista wa shirika COLU ni mwalimu wa dini mbali na majukumu mengine anaweza kufundisha watu elimu ya dini hivyo wawatumie ipasavyo katika kueneza injili ya bwana.
Askofu wa Jimbo Katoliki Tanga Mhashamu Anthony Banzi amewataka watawa kutambua kuwa nadhiri zao walizoziweka kwa Mungu ziwe ni sala ya kila siku . Masista waliofikia hatua hiyo wajitahidi kufanyakazi kwa umoja na misingi ya shirika .
Askofu Banzi amewakumbusha masista waliofikia hatua hiyo kutambua kuwa walitoka mbali, wapo mbali na  wanaenda mbali hivyo wanahitaji msaada wa Mungu kupitia sala zao.
 “Sisi tunawaombea kwa Mungu katika yale mnayosimamia kwani hapo mlipofika mmetoka mbali na mnakwenda mbali na kila mtu na maisha yake anapaswa kuheshimu nadhiri alizomuwekea Mungu kwa nafasi yake na iwe sala ya kila siku,” amesema Askofu Banzi


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU