Polisi wajipanga kudhibiti uhalifu msimu wa Krismas

Na Erick Paschal,Dar es Salaam.
Kuelekea sikukuu za mwisho wa mwaka Jeshi la Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam limeimarisha ulinzi katika maeneo yote ya jiji la Dar es Salaam,hususani katika taasisi mbalimbali za fedha (benki),maduka ya kubadilishia Fedha za kigeni na sehemu zenye mkusanyiko wa maduka mengi .
Akizungumza na wandishi wa habari Jijini Dar es Salaam Kamanda wa Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam SACP Lazaro Mambosasa amesema kuwa kipindi hiki cha kuelekea mwisho wa mwaka kumekuwa na baadhi ya watu ambao hujitafutia kipato kisicho cha halali kwa kufanya vitendo vya kiuhalifu,hivyo kutokana na hali hiyo jeshi la Polisi Kanda maalumu limejipanga kikamilifu kuhakikisha kwamba hakuna tukio lolote la uhalifu litakalojitokeza.
Kamanda Mambosasa alizidi kuongezea kwa kuwataka wanachi wasiwe na hofu pindi watakapoona  idadi kubwa ya Askari wakifanya doria katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam  na badala yake watoe ushirikiano kwa kutoa taaarifa za wahalifu.
Wakati huo huo Jeshi la Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam wamefanikiwa kukamata vipande 20 vya meno ya tembo vyenye thamani ya milion 87.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu Lazaro Mambosasa amebainisha kuwa, awali walipokea taarifa kuwa kuna watu wanaojihusha na biashara hiyo ya nyara za serikali,ndipo polisi waliweka mtego na kufanikiwa kukamata watuhumiwa watatu wakiwa na vipande hivyo,watuhumiwa ho wanaendelea kuhojiwa kwakushirikiana na maofisa wa maliasili na utalii na upelelezi ukikamilika watapelekwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU