Maisha ya mtawa ni kusali-Askofu Msonganzila asema

Na Veronica Modest Musoma.
Askofu wa Jimbo Katoliki  Musoma MichaeL Msonganzila amewakumbusha watawa kuwa watu wa sala, ili kujiweka karibu na Mwenyezi Mungu kama wito wao unavyotaka.
Askofu  Msonganzila ameyasema hayo Desemba 8 mwaka huu, wakati wa Misa Takatifu ya kuweka nadhiri za kwanza, za daima na jubilei ya miaka 25 na 50, kwa masista wa shirika la Moyo safi wa Maria  Afrika katika Kanisa la Novisiati lilopo Makoko,Jimboni humo.
 “Msiache kumbipu Mungu kupitia sala, yeye yupo kila sehemu ukimbipu tu anajipu wakati huo huo au anaweza kuchelewa kidogo kukujibu kwani hujibu kwa wakati.
Maisha yenu ya utawa yanahitaji majitoleo ya sala, kuwaombea watu, kuiombea dunia na kujiombea ninyi wenyewe,”amesema Askofu Msonganzila.
Amewaomba wazazi pia kuwaombea watawa wote wa kike na wa kiuume ,ili kupata nguvu katika wito wao,kwa kuwa peke yao hawawezi .
Mama Mkuu wa shirika hilo Sista Maria Lucy Magumba amewashukuru Masista hao kwa kuamua kumutumikia Mungu katika maisha yao yote, licha ya changamoto mbalimbali walizokumbana nazo katika maisha ya utawa,na hata wale walioweka nadhili za kwanza kwa kuamua kumtumikia Mungu katika maisha yao.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU