Mpeni Mungu nafasi ya kwanza-Ask. Ruwa’ichi

Na Erick Paschal
WAKRISTO wakatoliki nchini wameaswa kumpa Mungu nafasi ya kwanza kwa kuwa hakuna anayejua siku wala saa atakayoitwa na Mungu.
Wito huo umetolewa na Askofu Mkuu Yuda Thadei Ruwa’ichi wakati wa homilia yake kwenye adhimisho la ibada maalumu ya Misa Takatifu ya kumuombea marehemu Askofu Mstaafu Nestor Timanywa wa Jimbo Katoliki Bukoba aliyefariki Agosti 28, 2018 katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando.
Askofu Ruwa’ichi amesema kuwa Yesu anawaasa waamini wawe tayari na wito wa kuwa tayari unapaswa kupokelewa kwa uzito mkubwa. Ameongeza kuwa mara nyingi mwanadamu anapokuwa na afya nzuri anasahau kuwa kuna kifo na kuwa anapaswa kutoa hesabu kwa Mungu kwa kuwa uhai siyo mali ya binadamu, bali ni mali ya Mungu.
Amebainisha kuwa Mungu ndiye aliye hai, na uhai kwake siyo kitu cha kupewa na uhai ni hulka yake na kwamba binadamu wapo hai kwa sababu ya huruma yake na kwa kutambua hilo ni muhimu kumpa Mungu nafasi ya kwanza, kila dakika ya maisha ya kila mmoja.
Adhimisho hilo maalumu la kumwombea Marehemu Askofu Timanywa lililofanyika katika Kanisa Kuu la Epifania Bugando, liliongozwa na Askofu Mkuu Ruwa’ichi na lilihudhuriwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dodoma Mhashamu Beatus Kinyaiya na Askofu wa Jimbo Katoliki Geita Mhashamu Flavian Kassala.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU