Ask. Shao: Lazima tujifunze kusamehe

WAKRISTO nchini wametakiwa kuwa na huruma  na kujifunza kusamehe ili kuendeleza  amani na upendo uliopo baina yao na waamini wa dini nyingine.

Hayo yameelezwa na Askofu wa Jimbo Katoliki Zanzibar Mhashamu Augustino Shao wakati akifunga maadhimisho ya Mwaka wa Yubilei ya Huruma Ya Mungu visiwani Zanzibar 

Amesema kuwa ni vyema wakristo wakawa na huruma bila ya kuweka malipizi  au visasi kutokana na mambo mengi yaliyotokea ikiwemo kuuawa mapadri huku wengine wakijeruhiwa.

Hata hivyo Askofu Shao amesema kuwa wakristo wasamehe kwa moyo wa upendo bila ya kuweka kinyongo chochote katika nafsi zao ili kudumisha amani, upendo na utulivu katika visiwa vya Zanzibar.

Pia amebainisha kuwa upendo  na utulivu ni njia mojawapo ya kudumisha amani nchini  na  ya kuleta maendeleo hivyo hakuna budi kuienzi na kuitunza.

Wakati huohuo Askofu Agustino Shao ametoa mafunzo kuhusu mafuta ya upako wa wagonjwa kwa kubainisha kuwa mafuta hayo si ya wagonjwa tu bali ni kwa wakristo  wenye kubatizwa na wenye ndoa ya kikristo.

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU