Askofu Ruzoka awafunda waseminari waliohitimu Falsafa Kipalapala

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Tabora Mashamu Paul Ruzoka amwewaasa Mafrateri wa seminari Kuu Ya Mtakatifu Paulo Mtume Kipalapala kuwa waaminifu kwa Neno la Kristo na kumfuata Kristo kwa kuishi maisha ya ufukara na kukaa mbali na mali za dunia.
Rai hiyo ameitoa hivi karibuni katika Kanisa la seminari hiyo alipokuwa akitoa mahubiri yake yaliyolenga kumshukuru Mungu kwa neema nyingi alizowajalia mafrateri wa mwaka wa nne waliohitimu malezi yao seminarini hapo.
Akizungumza wakati wa Misa Takatifu Askofu Mkuu Ruzoka amewahimiza mafrateri hao wanaoenda kufanya utume wao katika sehemu mbalimbali za majimbo ya Tanzania kuishi yale walioyapata wakati wa malezi yao . “ Nendeni mkatoe harufu nzuri ili kwa wale mtakaowahudumia wamuone Kristo kupitia nyie”, Askofu Ruzoka amesema.
Aidha katika mahubiri yake Askofu Ruzoka amewaomba mafrateri wahitimu kujua sasa wameongezeka kimo na ufahamu hivyo hawanabudi kutumia elimu na maarifa waliyoyapata kwa faida ya Kanisa na wanapaswa kuhakikisha kundi la waamini linaongezeka.
Pia ameelezea wajibu wa kwanza wa wahitimu hao ni kuhakikisha wanahamasisha miito ya Upadri na utawa popote watakapokuwa kwani uhai wa Kanisa unategemea sana idadi wa vijana walioko katika seminari zetu majimboni. 
Aidha amewataka mafrateri hao wahitimu kutoa huduma yao kwa bidii, upendo na huruma kwa wote wataokutana nao katika mwaka wao huo wa uchungaji na baadae kama mapadri.
Amewataka kutumia ukomavu na busara kwani wanakokwenda hakuna uzio kama huu wa seminari bali wawe wakomavu na watu wenyekupima mambo.
Sambamba na kumshukuru Mungu pia katika Adhimisho la Misa Takatifu, Gambera wa Seminari hiyo Kuu Mh. Hermani Kachema alithibitishwa kuwa Gambera wa Seminari ya Kipalapala na kuendelea na utume wake ambao alishauanza tayari.
Mara baada ya Misa Takatifu ilifuata michezo na burudani mbalimbali ukumbini iliyohudhuriwa na wageni toka parokia mbalimbali za jimbo kuu Tabora.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU