Ask. Minde: Watoto wanaopelekwa seminari waandaliwe kiroho

Askofu wa Jimbo Katoliki Kahama Mhashamu Ludovick Minde ALCO/OSS ametoa wito kwa wazazi na walezi kuwa  wanapaswa kuwaandaa kiroho na malezi ya wito watoto wanaowapeleka kujiunga na seminari.
Wito huo ameutoa wakati wa Misa Takatifu ya Sherehe ya Seminari ndogo ya Malkia wa Mitume, Ushirombo  iliyoambatana na ufunguzi wa Bwalo la kulia chakula la seminari hiyo.
Askofu Minde amesema katika mambo ya Mungu yanapaswa kuongozwa na Roho Mtakatifu kuanzia kwenye familia.
Familia zidumu katika maisha ya uongofu, sala na kuwaandaa watoto kwa miitombalimbali ukiwemo wito wa upadri hata kabla hawajajiunga na seminari.
“Tusifanye mambo peke yetu tumuombe  Mungu atuongoze katika maisha na mipango yetu kwa kufaata mafundisho ya Kanisa.
 “Tunapoandaa  mambo yetu tusiongozwe  na jazba hatuwezi kuwa na mafanikio mazuri kwenye maisha yetu kama hatumshirikishi Mungu,” amesema Askofu Minde.
Amewataka waamini  kuomba hekima  ya Mungu kwa moyo wa sala amabazo zitafanikisha mipango yao.
Askofu Minde amesema  kuwa, Seminari ya Malikia wa Mitume iliyopo katika Parokia ya Bikira Maria Msaada wa Daima , Ushirombo ilikuwa inakabiliwa na sehemu ya kulia chakula kwa sasa kukamilika kwa bwalo hilo kumewaondolea adha hiyo waseminari hao.
Aidha katika misa hiyo kulifanyika harambee ya kuchangia seminari hiyo na jumla ya sh milioni 26.1 zilipatikana ambapo askofu Minde amewashukuru wazazi na walezi kwa kupeleka watoto wao kusoma hapo na kuwapongeza waamini wote waliojitoa kuchangia.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU