‘Wakatoliki ishini ukatoliki wenu’

Na Ivetha Kimburu, Iringa
WAAMINI wa Kanisa Katoliki wametakiwa kuishi maisha yaliyo mema katika Familia, Jumuiya , mitaa yao pamoja na jirani zao, ili Mwenyezi Mungu aweze kuidhihirika ndani mwao kila siku za maisha yao.
Hayo yameelezwa na  Makamu wa Askofu wa jimbo Katoliki la Iringa ambaye pia ni Paroko wa Parokia ya Ifunda Padri, Vicent  Mwagala wakati wa mahubiri yake kwa Waamini wa Parokia hiyo wakati akiadhimisha Sadaka ya Misa Takatifu ya kupaa Bwana.
Padri Mgwagala amesema kuwa, Mungu kamwe hawezi kujitenga nao na daima yuko kati yao kupitia Roho Mtakatifu ,ambaye anawaangazia ili Kristo aliyepaa Mbinguni aendelee kuishi ndani yao, kwani katika Kristo Waamini Wote wanatumaini kuufikia ufamle wa mbingu.
Ameongeza Kuwa zawadi ya Roho Mtakatifu kutoka kwa Mungu inawasaidia Waamini kutambua kuwa, wao wameunganika na Kristo aliyekichwa cha Kanisa, na kupitia kwake ndipo nao wataweza kufika mbinguni kwa Baba, lakini ili waweze kufika huko ni lazima wajibidishe.
Aidha Padri Mwagala ameeleza kuwa, Waamini wanapaswa kutambua kuwa wao ni tabernakulo pale wanapompokea Yesu Kristo wakiwa katika hali iliyo njema, kwani Yesu Kristo anaingia ndani mwao mzima na Mungu kweli, na hivyo wanatakiwa kuwaka daima moto wa mapendo, kama vile taa ya milele inavyowaka mbele ya Yesu wa Ekaristi.
Padri Mwagala amehitimiha mahubiri yake kwa kuwata, kuendelea kumuomba Mama Bikira Maria ili awe msaada kwao, na pia aendelee kuwaombea kwa mwanae, ili waweze daima kutambua uwepo wake  katika neno lake, huku nawao wakikubali kujitoa sadaka katika kuwasaidia wale wote wanaohitaji msaada wao.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU