Posts

“Majimbo yote yawe na tovuti”

Image
  KURUGENZI ya Mawasiliano ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) imeshauriwa kuhimiza matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano katika majimbo yote ili kuweza kuwafikia watu wengi zaidi na kupanua wigo wa Mawasiliano. Akizungumza na wakurugenzi wa Mawasiliano Jamii kutoka baadhi ya majimbo Katoliki Tanzania katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino (SAUT) kwenye Semina juu ya matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama), pia mbinu za Mawasiliano, Mratibu wa Mawasiliano Jamii wa Umoja wa Wanachama Mabaraza ya Maaskofu Katoliki Afrika Mashariki na Kati (AMECEA) Padri Chrisantus Ndaga amesema Kanisa Katoliki bado lina changamoto katika matumizi ya mitandao ya kijamii hususani tovuti za majimbo. Padri Ndaga ameyashauri majimbo yote Katoliki nchini Tanzania kufungua tovuti na mitandao mingine ya kijamii ili kutanua wigo wa Mawasiliano ndani na nje ya majimbo wakati akiwahimiza wakurugenzi wa Idara za Mawasiliano Jamii majimboni kuwaendeleza kitaaluma wa...

Wanadiplomasia wa Vatican ni madaraja kati ya Papa na Makanisa mahalia

Image
Taasisi ya Kidiplomasia ya Kanisa Katoliki ni mahali ambapo wawakilishi wa Vatican sehemu mbali mbali za dunia wanafundwa ili kuwa ni madaraja muhimu kati ya Kanisa la Kiulimwengu na Makanisa mahalia. Hawa kimsingi ni wawakilishi wa Baba Mtakatifu kwa familia ya Mungu sehemu mbali mbali za dunia. Ijumaa, tarehe 26 Mei 2019, Baba Mtakatifu Francisko alitembelea Taasisi ya Kidiplomasia ya Kanisa na kushiriki pamoja na familia hii katika sala, tafakari, chakula pamoja na kushirikishana furaha, matumaini na changamoto katika maisha na utume wa Kanisa la Kiulimwengu. Jumuiya hii ambayo kwa mwaka huu inaundwa na Mapadre 33 kutoka sehemu mbali mbali za dunia, imeonja kwa namna ya pekee, utu na ubinadamu; ukristo na upendo wa kibaba kutoka kwa Papa Francisko anayewachangamotisha daima kujiandaa kuwa kweli ni madaraja, mashuhuda na vyombo vya majadiliano kati ya watu wa Mataifa! Wanapaswa kutambua kwamba, wao ni madaraja muhimu sana kati ya Khalifa wa Mtakatifu Petro na Makanisa mahalia; J...

Maaskofu Kanisa Katoliki Kanda ya Magharibi wapiga kambi jimboni Sumbawanga.

Image
Maaskofu wa Kanisa Katoliki Kanda ya Magharibi wamepiga kambi ya siku tano jimboni Sumbawanga kwa ajili ya kujadili mipango ya kichungaji na maendeleo ya utume katika kanisa Katoliki Kanda ya Magharibi . Wakiongoza na mwenyeji wao Mhashamu Askofu Damian Kyaruzi wa Jimbo Katoliki la Sumbawanga, wengine ni Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Tabora Mhashamu Askofu Paul Ruzoka na Askofu Gervasi Nyaisonga wa Jimbo Katoliki Mpanda. Wengine ni Askofu Joseph Mlola wa Jimbo Katoliki Kigoma na Askofu Rudovik Minde wa Jimbo Katoliki Kahama ambayo inajumuisha majimbo matano likiwemo Jimbo Kuu Tabora. Akiwapokea maaskofu hao, mwenyeji wao Askofu wa Jimbo Katoliki Sumbawanga Mhashamu Damian Kyaruzi amesema kuwa maaskofu hao wanakutana metropolitan ya Tabora ambapo waliazimia kuwa kila mwaka kwa pamoja watakua wakizungukia majimbo yote kwa lengo la kufanya mikutano yao na kufanya shughuli za kichungaji katika majimbo na maazimio hayo yanaanzia katika Jimbo Sumbawanga kuanzia tarehe 25 May had...

MAGAZETINI LEO JUMATATU MEI 29

Image

REQUEST FOR PROPOSAL FOR EXTERNAL AUDIT SERVICES

CATHOLIC SECRETARIAT  TANZANIA EPISCOPAL CONFERENCE P.O BOX 2133 PHONE 022/2851075-9                022/2850047-8 FAX 022/2851133;            022/2850427 E-Mail info@tec.or.tz DAR ES SALAAM TANZANIA 18/May/2017 Department:  SEC - GEN Reference:   TEC/F&P/2/2017 REQUEST FOR PROPOSAL FOR EXTERNAL AUDIT SERVICES The Tanzania Episcopal Conference (TEC) is a permanent institution which was established since 1950s. TEC is the Assembly  of Catholic Bishops of Tanzania whereby according to the norms of law, certain pastoral functions are jointly exercised on behalf of Christ's faithful in view of promoting that greater good which the Church offers to all people especially through forms and programs of the apostolate which are fittingly adapted to the circumstances of our time and country. TEC desires to receive proposals for the selection...

‘Mauaji Kibiti kipo kilichojificha’ Ask Rwoma

Image
n   Na Pascal Mwanache K UFUATIA mfululizo wa mauaji ya viongozi wa serikali za mtaa na polisi yaliyojiri katika maeneo kadhaa ya Mkoa wa Pwani, Askofu wa Jimbo Katoliki Bukoba Mhashamu Desderius Rwoma amesema kuwa serikali haina budi kuweka nguvu katika kubaini walio nyuma ya matukio hayo. Askofu Rwoma amesema kuwa bila kujua nani na malengo ya matukio hayo serikali inaweza kudhani inapambana na mtoto mdogo kumbe nyuma ya pazia kuna mtandao mkubwa wenye malengo yasiyofahamika. “Tuweke nguvu kujua ni nani anafanya matukio haya, lengo lake ni nini na akina nani wanaounga mkono. Bila kujua hili tunaweza kudhani tunapambana na mtoto mdogo kumbe siyo” ameeleza Askofu Rwoma katika mahojiano maalum na Gazeti hili. Aidha ameshauri kufanywa uchunguzi wa kina ili kubaini aliye nyuma ya matukio haya ambayo yanahatarisha amani na usalama wa watanzania na hata serikali.Pia Askofu Rwoma ametoa wito kwa wananchi wa maeneo yaliyokumbwa na mauaji hayo kushirikiana na serikali katika ...

Wataliki na watalakiwa hawajaruhusiwa kupokea Ekaristi

Image
n   Na Sarah Pelaji, Dar es Salaam K UMEKUWEPO na uvumi katika mitandao ya kijamii kuwa Baba Fransisko kupitia waraka wake wa Furaha ya Upendo (Amoris Laetitia) ameruhusu wataliki na watalikiwa ambao wameshafunga ndoa nyingi (mfano ya kiserikali), kupokea Ekaristi. Uvumi huo sii kweli. Baba Mtakatifu amesisitiza kuwa watu hao wanapaswa kusaidiwa na Kanisa ili waweze kufahamu mpango wa Mungu juu yao. Hayo yamefafanuliwa na Tume ya Tume   ya Sheria za Kanisa ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania T.E.C. Mwenyekiti wake akiwa Askofu Rogathy Kimaryo, Makamu Mwenyekiti Askofu Michael Msonganzila na Katibu Mtendaji wa Tume hiyo Padri Henry Mchamungu mwalimu katika Seminari ya Mtakatifu Karoli Lwanga Segerea jijini Dar es Salaam. Tume hiyo imefafanua kwa waamini wote pamoja na makleri kuelewa kuwa, Baba Mtakatifu katika nyaraka hiyo alisema; “Katika kuangalia namna ya kukabili uchungaji kwa watu waliofunga ndoa za kiserikali, kwa wale waliopeana talaka na kuingia kat...