Wazazi waaswa kusaidia Utoto Mtakatifu kuinjilisha
WAZAZI na walezi kote nchini wametakiwa kujitoa kwa kila hali na mali kuwasaidia watoto kushiriki matamasha ya kiroho, kongamano na hija za Utoto Mtakatifu, ikiwa ni sehemu ya malezi kwa mtoto. Akitoa homilia katika Misa Takatifu kigango cha Mbutu Parokia ya Kimbiji Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam Paroko Msaidizi wa Parokia hiyo Padri Justus Lugayimkam amewakumbusha na kuwataka wazazi na walezi wote kutambua kuwa, jukumu la kulea Watoto wa Utoto Mtakatifu, lipo mikononi mwao na mtoto anapokua katika malezi ya dini humfanya awe mwenye heshima na mchamungu. Amesema wapo walezi ambao jukumu la Utoto Mtakatifu wamewaachia walimu jambo linaloleta ugumu kwa walimu pindi inapotokea watoto wanahitaji kushiriki katika matamasha mbalimbali . “Watoto wanahitaji mchango wa kifedha ili waweze kushiriki matamasha na watoto wenzao kutoka katika map...