Viongozi wa dini watakiwa kulinusuru Taifa

Na Rodrick Minja, Dodoma
MWENYEKITI wa Jumuiya ya Maridhiano Tanzania Alhaji Ibrahim Molel amewataka viongozi wa dini kulisaidia taifa katika kuliletea maendeleo ya kiuchumi, badala ya kutofoautina na kupigana vijembe.
Alhaji  Molel amewataka viongozi hao kuwa na umoja pamoja na kuvumiliana katika imani ili waweze kusonga mbele na hatimaye kuliwezesha taifa kufikia malengo yake ya uchumi wa viwanda.
Mwenyekiti huyo amesema hayo  wakati alipokuwa akifungua kikao cha elimu elekezi na namna ya kuongoza katika mikoa  na wilaya na jinsi ya kueneza maridhiano  kwa kila eneo kwa  viongozi  kutoka madhehebu mbalimbali ya dini waliotoka mikoa ya Tanzania  Bara kilichofanyika jijini Dodoma hivi karibuni
Amesema kuwa viongozi hao badala ya kupigana vijembe na kushindwa kusameheana watumie muda huo kwa ajili ya kujenga nchi  kwa ajili ya maendeleo ya kiuchumi yatakayofaidisha kila mtanzania hapa nchini.
Akizungumza kwenye kikao hicho amewataka viongozi hao pia kuwa na mioyo ya upendo na amani huku wakivumiliana ili waende kwa pamoja na kudumisha amani iliyopo.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Maridhiano Tanzania Mchungaji  Oswald Mlaya amewataka viongozi hao kutojihusisha na siasa badala yake wajikite kwenye kuiombea nchi na uchaguzi ujao wa viongozi wa serikali ya vijiji mitaa na vitongoji unaotarajiwa kufanyika mwaka huu.
“Kama viongozi wa dini kujiingiza kwenye siasa na kama mnavyoona kwa baadhi ya nchi za wenzetu wanavyouana wakati sasa umefika kwa viongozi hao kuja kwa pamoja madhehebu na dini zote kuwa na kauli moja itakayotufanya  tusipoteze amani na umoja uliopo nchini kwetu” amesema.
Naye Mwenyekiti wa jumuiya ya maridhiano mkoani Dodoma Shekhe Abbakari  Omary  amesema, “Kimsingi chombo hiki kwa wakati tulionao ni muhimu katika nchi yetu hivyo niwataka watanzania kujiunga kuwa mwanachama .
Nchi yetu inahitaji malezi ya kiroho na hakuna mahali panapoweza kupatikana isipokuwa kwenye vyombo vyetu vya dini ikiwemo makanisa na misikiti ili tuwe pamoja. Tumeanzisha jumuiya itakayotuweka pamoja kwa lengo kudumisha amani  na kudumisha na wananchi wafanya shughuli zao,” amesema.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU