Ukeketaji, umasikini, ugomvi wa wazazi chanzo cha watoto kuzikimbia familia

Na Veronica Modest Musoma
Umasikini, ukeketaji  na kuvunjika kwa ndoa   katika  familia kumetajwa kuwa ndio chanzo cha watoto wengi kukimbia familia zao na kujikuta wanakuwa wa mitaani.

Pia hali hiyo imetajwa kuchangia watoto wengine kuzikimbia familia zao na kulelewa katika vituo vinavyowasaidia watoto  wenye mahitaji  maalum.
 Hayo yamesemwa na wasichana  15 waliohitimu mafunzo ya fani mbalimbali ya stadi za maisha wa kituo cha Jipe Moyo kilichopo katika Parokia ya Mwisenge Jimboni Musoma ambao walikimbia ndoa za utotoni, Ukeketaji, waliobakwa na kufanyiwa vitendo vya ukatili na hatimaye kukimbia familia zao na kulelewa na kituo hicho kwa zaidi ya maiaka miwili.
 Msimamizi wa Kituo hicho Sr Maria Annunciata Chacha amesema  kwa sasa kituo kina zaidi ya watoto 130 wanaohudumiwa na wanakabiliwa na upungufu wa chakula.
Hivyo ameiomba Serikali  kuwasaidia chakula walau  hata mlo mmoja kama ni mchana au usiku maana wanaelemewa na watoto baada ya idadi kuongezeka.
 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Musoma Fidelica Myovella amesema ni kweli kituo kinajitahidi sana kuwalinda watoto kwani wengi waliopo katika kituo hicho wanatoka katika mikoa mbalimbali na wilaya zote za Mkoa wa Mara.
Hivyo wao kama serikali watawasaidia hata kuwapatia mikopo ili waweze kuendelea na ujasiriamali pamoja kwa kuanzisha kikundi chao sambamba na kutoa elimu kwa jamii.
 Mkuu wa wilaya ya Musoma Dk Vicent Naano amesema wataangalia namna ya kusaidia kituo hicho ikiwa ni pamoja na kuwapatia mlo mmoja wa chakula,kuwasaidia cherehani kwa ajili ya ushonaji, na mahitaji mengine kwani alikuwa hajui kama  wana changamoto kubwa kiasi hicho.
Amewaomba wasimamizi wa kituo hicho kuanzisha fani mbalimbali kama ufundi wa ujenzi wa nyumba, umeme na kuchomelea vyumba (welding), ili kupanua wigo kutokana na watoto wanaokuja kituoni hapo kuwa na vipaji tofautitofauti,huku suala la upungufu wa chakula kituoni hapo akiahidi kwenda kulifanyia kazi.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU