Posts

KUELEKEA MAHAFALI YA 19: SAUT YAJIVUNIA ELIMU BORA

Image
CHUO KIKUU cha Mtakatifu Agustino (SAUT) cha jijini Mwanza kimeendelea kusifiwa kwa kutoa elimu bora hasa kwa njia ya vitendo kwa wananchi ndani na nje ya Tanzania. Hayo yamebainika zikiwa zimesalia siku chache kabla ya chuo hicho kusherehekea mahafali yake ya 19 tangu kuanzishwa kwake mwaka 1998. Afisa Uhusiano wa chuo hicho Living Komu akizungumza na gazeti la Kiongozi amesema kuwa SAUT ni chuo cha kujivunia kwa wanafunzi wote waliopita hapo kwa maana ni chuo kitoacho wanafunzi bora kitaaluma na kimaadili. ‘Ili uweze kutambulika na kuheshimiwa ni lazima uwe na nidhamu njema na pia taaluma iliyotukuka, hivyo kama chuo kinajitahidi na kimeweza kufanya kadri ya uwezo wake kuzalisha wanafunzi wenye vigezo bora vya kuuzika katika soko la ajira ya sasa na hata baadaye ndani na nje ya Tanzania,’ amesema Komu. Amewakumbusha wanafunzi wote ambao wanakwenda kuhitimu katika mahafali ya 19 kuwa ni vyema watumie elimu na nidhamu waliyofunzwa hapo chuoni na kuwa kioo kizuri ka...

TEC YAPONGEZWA NA SERIKALI UKUZAJI ELIMU NCHINI

Image
NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara Mhandisi Stella Manyanya amelipongeza Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania kwa juhudi, maarifa na busara kuamua kuwekeza katika sekta ya elimu hivyo kuwa chachu ya ukombozi wa Mtanzania. Waziri Manyanya ameyasema hayo kwenye mahafali ya kumi ya Chuo Kikuu Katoliki cha Ruaha (RUCU) yaliyofanyika hivi karibuni kwenye viwanja vya chuo hicho na kuhudhuriwa na Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Katoliki Ruaha, Askofu wa Jimbo Katoliki Njombe Mhashamu Alfred Maluma, wahitimu wa fani mbalimbali kutoka chuoni hapo na  wageni waalikwa kutoka sehemu mbalimbali. Manyanya amesema kuwa Kanisa Katoliki kupitia Baraza la Maaskofu limekuwa mdau mkubwa wa elimu kabla na hata baada ya Uhuru, pia mshiriki mkubwa wa Serikali katika kuchangia ukuaji wa Elimu nchini na siyo katika elimu peke yake bali hata katika afya na huduma nyingine za kijamii. “ Napenda pia kutumia fursa hii kulipongeza Kanisa Katoliki kwa juhudi kubwa hasa katika kukuza na...

KARDINALI PENGO AZINDUA PAROKIA MPYA MISUGUSUGU.

Image
ASKOFU Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo amewaongoza waamini wa Misugusugu na wageni waalikwa kutoka parokia tofauti za Jimbo hilo kwenye sherehe za kuzindua parokia mpya ya Mt. Polycarp Misugusugu, sanjari na uzinduzi wa nyumba ya mapadri iliyojengwa parokiani hapo pia usimikaji wa msalaba wa kumbukumbu juu ya kilima kilichopo pembezoni mwa parokia hiyo. Katika mahubiri yake kwenye ibada hiyo ya misa takatifu, Kardinali Pengo amesema kuwa kwa kiburi cha Adam na Eva maisha yetu yametuwia magumu lakini bado Mungu anatupenda kwa upendo wake mkuu kwetu, akamtuma   mwanaye Yesu Kristo aje kutukomboa kupitia kwa mama yetu Bikira Maria aliyekuwa mtii na mnyenyekevu mbele za Mungu, hivyo kila mkristo adumu katika upendo kila wakati. Kwa upande wake Mwenyekiti wa   Parokia hiyo mpya, Adolf Mrema amesema, ‘Ni furaha iliyopitiliza kwa hatua tuliyoifikia kwa sababu tutakuwa na uhakika wa kufanya adhimisho la Ekaristi Takatifu a...

CARITAS MBEYA YAWAWEZESHA MABINTI WALIOTELEKEZWA

Image
WITO umetolewa kwa wazazi na jamii  kwa ujumla kuwatia moyo na kuwapatia  stadi za maisha  ikiwemo elimu ya ujasiriamali wasichana wadogo wanaopewa ujauzito na kutelekezwa  badala ya kuwaacha wakikata tamaa ya maisha. Ushauri huo umetolewa  na mfuatiliaji wa vikundi vya mabinti walea pekee kutoka Idara ya  CARITAS na Maendeleo, Jimbo Katoliki Mbeya anayeshughulikia maeneo ya Jiji la Mbeya, Magdallena Mwashala  alipokuwa akizungumza na KIONGOZI  mara baada ya kumtembelea mmoja wa mabinti walea pekee kujua maendeleo yake katika maeneo ya Tambukareli, Kata ya Itezi jijini Mbeya. Magdallena  amesema kuwa msichana Jane Ndangali  ni miongoni mwa wanakikundi cha Amka ambaye  alijikuta amejiingiza katika mahusiano na kuzalishwa watoto wawili  na baadaye kutelekezwa na mwenzi wake, lakini  baada ya kuhamasishwa kujiunga katika kikundi amefanikiwa kupewa mafunzo mbalimbali ya ujasiriamali, utunzaji wa fedha, kuishi kat...