Askofu Ngalalekumtwa ataka watawa kuiishi Injili


ASKOFU Tarcisius Ngalalekumtwa wa Jimbo Katoliki Iringa amewataka watawa kuwa vielelezo vya utakatifu na Injili ili wawe mfano kwa wanadamu.
Askofu Ngalalekumtwa amesema hayo katikati ya juma wakati wa kuweka nadhiri za kwanza kwa wanovisi 24 wa Shirika la Mtakatifu Teresia Mtoto Yesu Jimboni humo.
Wanovisi hao wametoka   majimbo mbalimbali ya Kanisa Katoliki nchini na kati yao watatu wametoka nchi ya Haiti.
Misa hiyo imefanyika kwenye kanisa la Moyo Mtakatifu wa Yesu Parokia ya Tosamaganga na kuhudhuriwa na mapadri, watawa wa kike na kiume pamoja na waamini wenye mapenzi mema kutoka ndani na nje ya Jimbo Katoliki Iringa.
Askofu Ngalalekumtwa amesema kwamba ikiwa watawa hao watakuwa ni vielelezo vizuri watawashawishi na wengine kuiga maisha yoa.
Amesema kuwa, wanatakiwa kuwa mfano wa kuigwa na anawaombea ili waweze kuzingatia ukweli wa majitoleo yao.
“Tunawaombea Kristo na Mama Bikira Maria aliye mfano wa mabikira, na Mtakatifu Teresia aliyemsimamizi wenu awasimamie katika utume wenu” amesema askofu Ngalalekumtwa.
Aidha askofu Ngalalekumtwa amesema kuwa, popote pale Kanisa litakapowahitaji sehemu yoyote wapate kuenenda vile Kristo anavyotaka.
Askofu Ngalalekumtwa amewataka pia waamini wote kuwaombea watawa hao, na pia watambue kwamba wanahitaji upendo wao, sala zao ili waweze kuviishi  viapo vyao kwa uaminifu.

“Kumfausa Kristo ni kazi ngumu yataka Neema ya Mungu, likiwepo Kanisa, shirika na Ulimwengu wahitaji watawa wenye msimamo unaoleweka,” amesema.

Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU