Serikali yapokea ripoti ya utafiti wa viongozi wa dini kuhusu afya


Sarah Pelaji na Rodrick Minja, Dodoma
Serikali yapokea ripoti ya Viongozi wa dini kuhusu hifadhi ya jamii kwenye sekta ya afya Octoba 4 mwaka huu katika Mkutano wa Viongozi wa dini mbalimbali uliofanyika katika Ukumbi wa Mt. Gaspari Dodoma.
Akipokea Ripoti hiyo kwa niaba ya serikali Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii Dokta John Jingu amebainisha kuwa jukumu kubwa la serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dokta John Pombe Magufuli ni kuhakikisha kuwa msisitizo mkubwa ni kuwahudumia walio wanyonge.
Amesema kuwa viongozi wa dini wamekuwa wakihubiria waamini wao juu ya huduma kwa wanyonge na maskini zaidi pamoja na kuwasaidia walio wadogo.
“Serikali yetu tangu ipate uhuru imekuwa ikisisitiza hivyo wakati iliposisitiza kupiga vita maadui watatu ambao ni ujinga, maradhi na umaskini ilikuwa inamaanisha hivyo” aliongeza Dokta Jingu.
Hata hivyo amesema kauli ya Rais Magufuli ya kuwa yeye ni Rais wa wanyonge ina maana kuwa serikali yake ni ya wanyonge hivyo mkazo ni kuwahudumia wanyonge ndio maana serikali imeweka idara maalumu ya kuwashughulikia walio wanyonge ambayo Wizara yake ni Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto.
Dokta Jingu amesema kuwa Wizara yake kupitia sera yaTaifa ya  Afya ya mwaka 2007 na sera ya Afya ya Wazee ya mwaka 2003  imeweka mkazo katika kuwahudumia walio wanyonge na hususani Wazee ambao wana umri kuanzia miaka 60 na kuendelea kupatiwa matibabu bure bila ya malipo.
Amesema kuwa katika kutekeleza sera na miongozo mbalimbali ambayo wamekuwa wakipata katika kuhudumia makundi hayo madogo wamekuwa na ushirikiano na tamisemi katika kuona ni namna gani ambayo wanaweza kutekeleza sera hiyo lakini pia na idara ya kuboresha afya ya ustawi wa jamii.
Amesema katika kuhakikisha hayo wamefanya zoezi la kutambua wazee katika halmashauri zote nchini na kuwapatia vitambulisho vya matibabu bila ya malipo ambapo hadi kkufikia septemba 2018 wamegundua uwepo wa wazee milioni moja laki nane na hamsini elfu na mia sita na ishirini na mbili huku wanaume wakiwa ni laki nane nane na arobaini na saba elfu mia tisa hamsini na tano na wanawake wakiwa ni milioni moja na elfu mbili mia sita sabini na saba wametambuliwa na kati yao laki saba hamsini na nne elfu mia sita sitini na saba wamepatiwa vitambulisho vya matibabu bila malipo.
Aidha Dokta Jingu amesema kuwa serikali inaendelea kuhakikisha kuwa wazee wote ambao hawana uwezo wanapatiwa matibabu hayo lakini kumekuwapo na changamoto katika eneo hilo ambapo baadhi ya watoa huduma wamekuwa wakiwanyanyapaawazee hao  na kwa kuliona hilo siku ya wazeenduniani kwa hapa nchini Tanzania ilivyoadhimishwa Kitaifa Mkoani Arusha Oktoba Mosi mwaka huu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Mheshimiwa Ummy Mwalimu alitoa maelekezo na maagizo kwa wale wote ambao wanawanyanyapaa wazee washughulikiwe.
Amesema kuwa wao kama Viongozi wameahidi kulishughulikia suala hilo  na kwamba endapo mzee yeyote atakayenyanyapailiwa katika kituo chochote kile cha afya au hospitali anapaswa kubainisha jina la mhusika wa kitendo hicho na atoe taarifa mahali husika na wizara itachukua hatua stahiki.
Dokta Jingu amebainisha kuwa wizara kupitia NHIF na CHIF wamekuwa wakijitahidi kuboresha huduma za afya kwa watu wote.
“Hapa kuna changamoto kubwa ambapo kuna watu wanauwezo wa kupata huduma hizi lakini kwa njia moja ama nyingine wanakwepa ama hawajui umuhimu wa kujiunga na huduma hizo” aliongeza Dokta Jingu.
Hata hivyo amewaomba viongozi wa dini waliohudhuria uzinduzi wa ripoti hiyo kuendelea kuhamasisha wananchi kujiunga na mifuko inayotoa huduma za matibabu.
“Wakati NHIF inaanza baadhi ya watu waliona kuwa mfuko huo umelenga kuwachukulia wananchi fedha zao kumbe sio hivyo ndio maana tuliwaita watendaji na kuwaweka kitimoto lakini baada ya kupata vitambulisho hivyo na kuanza kutoa huduma faida imeonekana lakini kuna haja ya kufanya ulazima wa kuhakikisha kuwa kila mfanyakazi wa serikali anajiunga na mfuko huo wa NHIF” aliongeza.
Dokta Jingu amesema kuwa kwa sasa inabidi kuwepo na kulazimisha watu kujiunga na NHIF kwani wengi wanakuwa wakipinga bila ya kujua wanachopinga na baadae wanapogundua faida zake wanajilaumu.
Dokta Jingu amesema lengo la utafiti na mapendekezo yanayotoakana na utafiti sio kutoa mahitimisho isipokuwa ni kuchocvhea fikra ili tuzidi kufikiri zaidi na kushughulikia changamoto zilizopo.
Ripoti ya viongozi wa dini kuhusu hifadhi ya jamii kwenyesekta ya afya.
Akiwasilisha Ripoti  hiyo ya Viongozi wa dini Mtafiti katika Kamati ya Dini mbalimbali nchini Dr.nMoses Kulaba amesema kuwa, ripoti hiyo inajaribu kujibu swali, ‘ Tunaweza je kuongeza upatikanaji wa hifadhi ya jamii kwenye sekta ya Afya kwa kutumia mapato au fedha mapato ya ndani?
Amesema ripoti inaonyesha  Tanzania inaweza kuongeza au kugharimia  upatikanaji wa Bima ya Afya kwa Watanzania wote (Universal Health Coverage) kwa kutumia fedha za mapato yake ya ndani (Own tax sources) bila kutegemea ufadhili mkubwa kutoka nje. 
Ripoti imetazama hali ya sasa hivi ya upatikanaji wa Bima ya Afya kwa watanzania na haswa watu wa kipato cha chini
Imeangalia mafanikio na mapungufu ya kisera , ki takwimu na kibajeti  na changamoto za upatikanaji wa bima ya Afya kwa watanzania.


Inaendelea Uk. 8

Inatoka Uk. 4

Ripoti inapendekeza njia mbadala za muda mfupi na mrefu  zinazoweza kusaidia Serikali kugarimia watu au  kaaya masikini wapate bima Afya na kuongeza usajili wa idadi ya watu wenye Bima ya Afya kutoka asilimia 32 mpaka Asilimia 100 ifikapo 2025.
Tarifa zinaonyesha changamoto kubwa za kisera , ki mfumo na kifedha za upatikanaji wa bima ya Afya
Wakati wa kukusanya tarifa takwimu kutoka serikali zilionyesha kati ya hawa asilimia 32 asilimia 7- 8%  wamejiunga na Bima ya Afya  au (National Health Insurance Fund -NHIF), 23%  wamejiunga na Mfuko wa Bima ya Jamii ( Community Health Fund -CHF).  Na asilima  moja wamejiunga na Makampuni binafsi ya kutoa Bima za Afya. (National Health Insurance Funds (2017) Annual fact sheet 2016/2017, NHIF Dar es Salaam).
Tafsiri yake ni kwamba asilima 68 ya Watanzania wote hawana Bima ya Afya. Wakipata matatizo ya Afya wanalazimika kuingia mifukoni kulipia garama za huduma ya Afya.
Kati ya hawa asilimia 68 kuna asimila 40 wanaweza kuchangia malipo ya bima ya Afya lakini kuna asilimia 28 takribani ya watu kam 14.3 million  ni masikini sana na hawana uwezo kulipia bima ya Afya
Tafsiri yake ni kwamba bila msada  hawa wakipata matatizo ya Afya wanaweza kukosa matibabu na pengine hadi kufa.
Kwa kufanya mabadiliko madogo madogo sana kwenye sera za kodi mbali mbali serikali inaweza kabisa kupata pesa ya kulipia hawa asilimia 28 masikini na kutenga pesa   za kulipia  (matching funds) za wale asimila 40 ambao bado hawajajiunga.
Fedha hizi zinaweza kutokana na kuanzishwa utaratibu wa kutenga kiasi cha fedha kutoka vyanzo mbali mbali vya kodi (ring fenced revenues) kama sekta ya madini  na vyanzo vingine bila kuongeza kodi na kuelekeza pesa hizi kugharimia bima ya Afya.
Kwa  kulenga asilimia kugarimia asilimia 17 kila mwaka ya wananchi wote walio nje ya bima  serikali inaweza kuongeza upatikanaji wa bima kutoka asilimia 32 hadi 91 ndani ya miaka miwili na hadi asilimia 99 au 100 ifikapo 2025.
Uzoefu kutoka nchi nyingine unmeonyesha kwamba kwa kuthubutu kabisa na thamira ya makusudi   (national political and leadership will) inawezekana.
Kuna mahusiano kati ya Afya mbaya na umasikini na kuwekeza kwenye Afya ni mtaji (social investment) kubwa kwa nchi kwahiyo kuna haja kubwa sana ya kuangalia jambo hili kwa uzito huo na kuwezesha upatikanaji wa bima ya Afya haraka iwezekanavyo.
Kwa kufanya mabadiliko madogo madogo sana kwenye sera za kodi mbali mbali serikali inaweza kabisa kupata pesa ya kulipia hawa asilimia 28 masikini na kutenga pesa   za kulipia  (matching funds) za wale asimila 40 ambao bado hawajajiunga.
Pesa hizi zinaweza kutokana na kuanzishwa utaratibu wa kutenga kiasi cha fedha kutoka vyanzo mbali mbali vya kodi (ring fenced revenues) kama sekta ya madini  na vyanzo vingine bila kuongeza kodi na kuelekeza pesa hizi kugharimia bima ya Afya.
Kwa  kulenga asilimia kugarimia asilimia 17 kila mwaka ya wananchi wote walio nje ya bima  serikali inaweza kuongeza upatikanaji wa bima kutoka asilimia 32 hadi 91 ndani ya miaka miwili na hadi asilimia 99 au 100 ifikapo 2025
Uzoefu kutoka nchi nyingine unmeonyesha kwamba kwa kuthubutu kabisa na thamira ya makusudi   (national political and leadership will) inawezekana
Kuna mahusiano kati ya Afya mbaya na umasikini na kuwekeza kwenye Afya ni mtaji (social investment) kubwa kwa nchi kwahiyo kuna haja kubwa sana ya kuangalia jambo hili kwa uzito huo na kuwezesha upatikanaji wa bima ya Afya haraka iwezekanavyo
Kiasi gani cha fedha kinahitajika na kitoke wapi?
Dr. Kulaba amebainisha kiasi kinachohitajika kugarimia  asilimia 28  ya masikini wasio na bima ya afya kuwa  ni  shillingi 180 kama serikali ikiamua kulipa garama yote (elfu 60, 000) ya bima ya afya ya jamii iliyoboreshwa (iCHF) kwa kila kaaya. 
Lakini, kaaya hizo masikini wakichangia angalau elfu kumi kwa mwaka na serikali kuongezea elfu hamsini, garama ni yote kwa miaka mitano in billion150. 
Serikali inahitaji billion 127.2 ilikulipia kama mchango wake (matching fund) kwa wale asilimia 40 ambao wanauwezo lakini bado hawajajiunga lakini wanaweza kuijunga wakihamasishwa.
Kumbe serikali ikitenga  billion 277 leo au ndani ya miaka mitano inaweza kufikia asilimia 91 ya watanzania wote na bima ya afya ifikapo mwaka 2025 kwa kutumua fedha za mapato ya ndani .
Serikali inahitaji billion 290 ili kuwafikia asilimia miamoja ya watanzani wote (ikiwemo na wanolipiwa na makampuni binafsi) kupata bima ya Afya ndani ya miaka 5-6.
Ili kupunguza mzigo wa kibajeti serikali inaweza kulenga kufikia kaaya asimilia 17 kila mwaka kwa miaka mitano hadi sita.
Serikali inaweza kulipia  kaaya masikini (28 ya wananchi wote nchini) kwa kutenga asilimia 19 tuu kutoka kwenye vyanzo vya kodi mbali mbali.
Kiwango cha kodi kutoka kodi ya ongezeko ya thamani ni kidogo sana sawa na asilimia 0.15% kila mwaka na kufikia asilimia 0.9% in 2025.Viwango hivi ni vidogo  na vinawezekana .
Serikali ianzishe utaratibu wa kutenga asilimia ya kiasi kutokana na vyanzo vya kodi mbali mbali kama tulivyopendekeza hapo juu ili kulipia garama bima ya Afya (Health Insurance Coverage).
Serikali iwawezeshe kaaya masikini (asilimia28)  kupata bima  ya afya kwa kulipia elfu 50,000 huku kaaya zikichangia elfu 10,000.
Serikali itenge pesa za kutosha kuchangia kaaya asilimia 40 ambao wako kwenye sekta binafsi kama mchango (matching fund) wanapojiunga.
Kuna haja ya kuhamashisha wananchi wengi kujiunga na Bima za Afya.. Msistizo  tuelekeze kwenye vijana wajiunge kwa wengi.
Matatizo na changamoto za watoaji na utoaji huduma ya Afya chini ya mipango ya Bima Afya yatatutliwe mara moja. Kwa mfano, kuchelewesha malipo, kukosekana kwa dawa na wahudumu, nk
Kupunguza garama za uendeshaji wa mifuko ya Bima ya Afya na kuongeza kiwango cha pesa kinachofika kwenye vituo vya Afya
Viongozi wa dini wanapendekeza kuwepo kwa mfuko rasmi (National Sovereign Fund) ya Afya na utaratibu wa kupeleka pesa kwenye mfuko kutoka sekta nyingine kama madini ya Oil and Gas Fund.
Aidha ripoti imetoa majukumu kwa serikali na viongozi wa dini huku wakiitaka Serikali kufanya Mabadiliko ya kisera , kimufumo na utaratibu wa kikodi, Upatikanaji wa huduma na malipo kwa watoa huduma.
Viongozi wa dini wafanye Uhamasishaji wa wananchi Kutoa huduma kupitia vituo vyao vya afya Kufuatilia na tathmini ya upatikanaji wa huduma, ubora nk.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU