Balozi wa Baba Mtakatifu afanya ziara ya kichungaji Jimboni Musoma




Na Veronica Modest- Musoma
Balozi wa Baba Mtakatifu nchini Askofu Mkuu Marek Solczynski  amefanya ziara ya kichungaji kwa mara ya kwanza tangu kuteuliwa kwake,katika Jimbo  Katoliki  Musoma kuanzia Oktoba  02 hadi 09  mwaka huu.
Katika ziara hiyo Balozi huyo ametembelea maeneo mbalimbali ambapo Oktoba 02 alikuwa katika Parokia ya Kiabakari na aliongoza Ibada ya uzinduzi wa kituo cha Hija ya Huruma ya Mungu Kiabakari na kukipandisha kutoka hadhi ya Kijimbo hadi hadhi ya Kitaifa pamoja na kubariki Kikanisa (chapel)  cha Bikra Maria.
Ametembelea kliniki ya meno na macho katika kituo cha afya cha Blessed Pier Giorgio Frassati Kiabakari na kubariki wagonjwa.
Akiwa Parokiani hapo alikutakutana pia na mapadri ,watawa na waamini wa udekano wa Butiama.
Oktoba 03 Balozi huyo  akiwa katika Kanisa Kuu la Musoma alishiriki kusali Rozari Takatifu na waamini wa parokia hiyo na aliongoza  ibada ya Baraka Kuu na baadae alikutana na watawa na waamini  wa udekano wa Musoma .
 Oktoba 04 ametembelea ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara, baadae ameadhimisha Misa Takatifu  na katiak  Seminari ndogo  ya Makoko kisha kuwatembelea manovisi na kuwabariki masisita wazee na  wagonjwa katika nyumba yao iliyopo Makoko. Pia amefanya mazungumzo na masista wa shirika la  Moyo safi wa Maria Afrika .
 Oktoba 05,atatembelea Parokia ya Utegi ambapo atabariki wakristo na kubariki jiwe la msingi la nyumba mpya ya mapadri.
Kisha ataelekea Tarime ambapo atawabariki wakristu  na kubariki jiwe la msingi  la Kanisa jipya la parokia ya Tarime.
 Oktoba 06,atatembelea Parokia ya Mugumu na ataadhimisha Misa na kutoa Sakramenti ya ubatizo kwa watoto wachanga na kuwapa watoto Sakramenti ya  Komunyo ya kwanza kisha atabariki nyumba mpya ya masista,baadae ataelekea Fort Ikoma  Serengeti.
Oktoba 07 ,atasali Misa Takatifu  katika Parokia ndogo ya Serengeti(Fort Ikoma)kisha atakwenda Seronera.
Oktoba 8 ,atakuwa na Misa Bilila na katika Jumuiya ya Mt. Francis wa Assis  na wakristo wa eneo hilo,baadae ataelekea Serena,ambapo  atasali Misa katika Jumuiya ya Mtakatifu John Paul II.
Oktoba 09 ataondoka eneo la  Serengeti na kuelekea Mwanza .


Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU