Wazazi warithisheni watoto elimu-Askofu Nyaisonga asisitiza
Na Thompson Mpanji, Songwe WAAMINI wa Kanisa Katoliki wametakiwa kuwaendeleza watoto wao katika elimu ikiwemo na wao wenyewe kujiendeleza katika fani mbalimbali ili waweze kujiajiri kupitia mafunzo mbalimbali waweze kujitegemea. Elimu ndiyo hazina pekee na urithi mkubwa kwa familia na jamii kwa ujumla katika maisha ya sasa na ya baadaye. Ushauri huo umetolewa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Mbeya,Mhashamu Gervas Nyaisonga wakati wa homilia yake katika adhimisho la Ibada ya Misa Takatifu iliyofanyika katika Kanisa la Mtakatifu Francisco wa Asiz, Kigango cha Mkwajuni,Parokia ya Mwambani,jimboni humo. Walioshiriki ibada hiyo licha ya waamini wa parokia hiyo, walishiriki pia Wafanyakazi wa Hospitali ya Mwambani inayomilikiwa na Jimbo Kuu Katoliki la Mbeya, iliyopo katika Kigango hicho ambako Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Mbeya Mhashamu Gervas Nyaiaonga alifanya ziara ya kutembelea H...