Benki ya Mkombozi yafungua tawi Iringa
Na Getrude Madebwe, Iringa B enki ya Biashara ya Mkombozi imefungua tawi mkoani Iringa ikiwa ni utekelezaji wa mipango ya Benki hiyo kupanua huduma zake ili kuwahudumia wananchi kwa ukaribu. Akifungua tawi hilo, Askofu wa wa Jimbo Katoliki Iringa Mhashamu Tarcisius Ngalalekumtwa amewataka waamini wa jimbo hilo, wananchi na watu wenye mapenzi mema kuitumia Benki ya biashara ya Mkombozi ambayo imeanza kutoa huduma zake mkoani humo. Benki hiyo inatoa huduma mbalimbali za kibenki ikiwa ni pamoja na kutoa mikopo kwa vikundi, mtu binafsi, taasisi na mashirika mbalimbali. Tawi hilo la Iringa ni kati ya matawi 10 ya Benki hiyo lengo ikiwa ni kuenea nchi nzima. Awali, Askofu Ngalalekumtwa ameyabariki majengo ya Benki hiyo yaliyopo kwenye Chuo Kikuu cha Kanisa Katoliki cha Ruaha (RUCU) na amesisitiza umuhimu wa kuweka akiba kwenye benki. “Tulitamani sana kuidhisha lile ambalo tumeidhinisha leo hii, benki ambayo tumeishughulikia sasa imefunguliwa hapa kwetu, ni nafasi ya b...