Posts

Bweni lateketea, Biblia na Rozari pekee vyasalia

Image
Mwanafunzi wa Seminari ndogo ya St. Mary Mbeya akionyesha Biblia Takatifu iliyosalimika mara baada ya moto kuteketeza vifaa vilivyokuwa katika moja ya mabweni seminarini hapo hivi karibuni (Picha zote na Thompson Mpanji) Baadhi ya vifaa vilivyoteketea kwa moto lakini Biblia na Rozali zilikutwa salama Hata baada ya moto kuteketeza vifaa hivi, Biblia na Rozari vimekutwa salama θ Ni Seminari ndogo ya St. Mary Mbeya J ANUARI 21 mwaka huu zaidi ya  wanafunzi 52 wa Shule ya Seminari ndogo  ya St.Mary’s ya Mbalizi Jimbo Katoliki Mbeya  wamenusurika  kifo kutokana na ajali ya moto ulioteketeza bweni lote na vifaa vilivyokuwemo.   Aidha  tukio jingine la ajabu ni kutoungua kwa  Biblia  na Rozali Takatifu zilizokuwa zimehifadhiwa katika masanduku ya bati ya wanafunzi  licha ya vingine vyote na jengo kuteketea kwa moto.  Akizungumza na Gazeti Kiongozi, Gombera wa Seminari hiyo Padri Edwin Mwimba am...

Kanisa kujitoa rasmi kuchukua Hospitali ya Rufaa Kwangwa Musoma

Modest na Bertha Mayayi Musoma. I meelezwa kuwa kukosekana kwa hati miliki, thamani kubwa ya fidia, pamoja na kukosekana kwa wahisani wa ufadhili zimetajwa kuwa ni miongoni mwa sababu zilizosababisha Kanisa Jimbo Katoliki Musoma kujitoa rasmi kimaandishi juu ya ombi la kuchukua na kuendeleza Hospitali ya Rufaa Kwangwa ambayo kwa sasa inasimamiwa na serikali.           Hayo yamebainishwa na Askofu wa jimbo hilo Mhashamu Michael Msonganzila hivi karibuni wakati akichangia hoja katika kikao cha kamati ya ushauri ya Mkoa wa Mara (RCC) ambapo alikieleza kikao kuwa maazimio mengi ya kikao hicho kuhusu Kanisa kuendelea na ujenzi wa Hospital hiyo, yameshawasilishwa kwa maandishi katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mara. Askofu Msonganzila amesema kuwa, Kanisa lilifuatilia vielelezo muhimu vya umiliki halali wa hospitali hiyo ya rufaa kwa muda wa miaka miwili bila mafanikio yeyote ikiwa ni pamoja na kukosekana kwa hati miliki ya eneo husika kama ilivyoahidiwa na kutol...

Kanisa lafungua kitengo cha Magonjwa ya Mfumo wa Chakula Dodoma

Image
Minja-DODOMA. K anisa Katoliki hivi karibuni limefungua kitengo cha Magonjwa ya Mfumo wa Chakula (ENDOSCOPY) katika Hospitali ya Mtakatifu Gemma iliyoko Miyuji Dodoma. Wakati wa ufunguzi wa jengo hilo, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dodoma Mhashamu Beatus Kinyaiya ameiasa jamii kuwa na mwamko wa haraka kuchangia huduma za afya pale zinapohitajika ili kunusuru maisha ya watanzania. Pia iwe na mipango ya kudumu ya huduma za afya kwa maendeleo. Pamoja na hayo Askofu Mkuu Kinyaiya amesema ufunguzi wa kitengo hicho ni muhimu kwa wananchi wa Dodoma kwani wamekuwa wakisumbuka kwa muda mrefu na kuwataka madaktari katika Hospitali hiyo kuwa na moyo wa huruma katika kuwahudumia wagonjwa. Aidha amewasisitiza kulinda vifaa tiba katika kitengo hicho. Kwa upande wake Mganga Mkuu Msaidizi katika Hospitali hiyo Sista Dkt. Theodora Mwasu amesema kuwa,wazo la kuanzisha Hospitali hiyo lilikuwa ni kwa ajili ya kuwatibu masista wagonjwa na wazee ambapo kwa sasa hospitali hiyo inatoa hudum...