Mitandao isiwatenge na Mungu-Askofu Mstaafu awaonya vijana
MWENYEKITI wa jukwaa la Kikristo Tanzania, mkoani Mbeya, Askofu mstaafu John Mwela, amewaonya vijana wa kitanzania kuwa matumizi ya mitandao ya kijamii na kukua kwa sayansi na teknolojia kusiwatenganishe na Mungu. Askofu Mwela ameyasema hayo wakati akikabidhi misaada mbalimbali ya vyakula, nguo na mahitaji muhimu ikiwemo vifaa vya shule vilivyochangwa na wasamaria wema wa kikristo na kiislamu jijijini Mbeya na kuwasilishwa kwa Shirika lisilo la kiserikali la Sauti ya Mama Afrika(SAMAFO) akisema kuwa mitandao ya kijamii imekuwa ikiwaondolea vijana walio wengi hofu ya Mungu na kuiga matendo yasiyompendeza Mungu. Ametoa wito kwa shirika la Sauti ya Mama Afrika kuendelea kutoa elimu kwa jamii hasa vijana na familia majumbani kuwa wasimsahau Mungu kwani kwa sasa hali imekuwa ni mbaya kwa vijana walio wengi wamefikia hatua ya kuona kwamba Mungu yupo katika mitandao wanayoperuzi. Askofu Mwela amesema kwa sasa dunia ni kam...