Simanzi yatawala mazishi ya Pardi Andrew Lupondya
Maaskofu wa majimbo manne , mapadri , watawa na mamia ya waamini wameshiriki misa ya mazishi ya Padri Andrew Lupondya (33) na watoto watano wa shirika rafiki wa utoto wa Yesu (VIFRA) na mlezi wao Mama Judith Kajwahula (63 ) wa jimbo Katoliki Kahama waliofariki katika ajali ya gari. Ajali hiyo ilitokana na gari walilokuwemo kugongana uso kwa uso na roli aina ya fuso Disemba 24 na marehemu wamezikwa katika eneo la kiwanja cha kanisa kuu la Mtakatifu Karoli Lwanga parokia ya Kahama mjini. Misa ya mazishi imefanyika katika kanisa kuu la jimbo na imeongozwa na Askofu Fravian Kasala wa jimbo Katoliki Geita, pamoja na Maaskofu Liberatus Sangu wa Shinyanga, Joseph Mlola wa Kigoma na mwenyeji Askofu Ludovick Minde wa Kahama. Akihubiri katika misa hiyo Askofu wa jimbo Katoliki Shinyanga Liberatus Sangu amesema “Kifo ni fumbo la Kristo, alishinda maut...