Prof Makubi: Corona bado ipo wananchi msibweteke
MGanga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi
amewataka wananchi waendelee kuchukua
tahadhari juu ya maambukizi ya ugonjwa
wa covi 19 unaosababishwa na virusi vya corona.
Prof. Makubi ameeleza hayo hivi karibuni alipokuwa anazungumza na Gazeti Kiongozi kuhusu kile kinachosadikiwa
na jamii kuwa tayari kuna dawa ya corona.
“Ninachiotaka kuwaambia wananchi ni
kwamba, hakuna dawa ya corona. Mpaka sasa dawa haijapatikana nna ile tuliyoleta
kutoka Madagascar bado inafanyiwa uchunguzi kujiridhisha.
Wananchi hawa vijana na wale waishio
vijijini wanapaswa waelewe kuwa, virusi
vya corona havibagui umri wala mahali.
Vijijini corona ipo tena ni rahisi
kusambaa hasa kwenye minada na magulio. Hivyo waendelee kuchukua tahadhari kama
zinavyoelekezwa na serikali pamoja na
wataalamu wa afya ikiwemo WHO.
Amewataka wenyeviti wa Mitaa, Vijiji, kata
nk. kuweka mikakati ambayo itawasababisha wananchi waendelee na shughuli zao za kiuchumi.
“Kwa mfano minada inaweza kuongezwa kwenye
maeneo ambayo yako wazi. Mnada wa wawanyama peke yake, wa vyakula peke yake, wa
nguo nk.
Na kila anayeingia avae barakoa. Kwa watu
wa kijijini wanaweza kujitengenezea barakoa kwa kutumia vitambaa vya cotoni
vyenye leya mbili, wawe na maji na sabuni ya kunawa mikono na kuepuka kugusana.
Wakae umbali unaopendekezwa na wataalamu,” amesema.
Amewataka wananchi waepuke mikusanyiko
isiyo na maana na kama hakuna lazima ya kwenda kwenye mikusanyiko wananchi
watulie majumbani mwao.
“Ninawashukuru wananchi kwa kuonesha
juhudi ya namna ya kujikinga wengi wanavaa barakoa, wananawa mikono hivyo
waendelee hivyo hivyo maana hakuna dawa.
Kwenye baa
waweke maji, wahudumu wanawe, wateja wanawe
Meza ziwe mbalimbali viti kadhalika,”
amesema.
Amewataka wananchi kupuuza taarifa za
uongo zinazoenea mtaani kuwa kuna dawa ama kuwa ugonjwa huu hauui, na kwamba
vijijini wapo salama.
Ugonjwa huu upo na mpokee taarifa na maelekezo
kutoka kwa serikali, wizara ya afya na wataalamu wa afya tu. Msisikilize
porojo za mtaani,” amesisitiza.
Kwa upande wake Askofu wa Jimbo Katoliki
Rulenge Ngara Mhashamu Severine-Niwemugizi amewasisitiza waamini wa jimbo hilo
kufuata malekezo wanayopewa na serikali pamoja na wataalamu wa afya na
wasipuuzie kwasababu wapo waamini
wanaotunga maelekezo ya ugonjwa huo.
“Nina wasiwasi juu ya wananchi wanaoishi
vijijini kwani ugonjwa huu ukiingia kijijini kwa kasi wananchi wanafariki sana
kwani katika shughuli zangu za kichungaji nikipita mtaani ninaona vijiweni
wananchi hawana ile social distance(umbali kati ya mtu na mtu.
Wengine ukiwaambia kunawa mikono wanaona
ni matumizi mabaya ya maji kwani kwao
maji ni kama mali ghafi kwasababu ya ukosefu wa maji vijijini.
Amesema elimu vijijini bado inahitajika
kwa wananchi wa vijijini ambao wanauchukulia ugonjwa huu kwamba si wao,”
amesema.
Akieleza kufungua shughuli za ibada
kupitia barua yake ya kichungaji aliyoitoa hivi karibuni amewataka waamni wake
kuendelea na shughuli za ibada kwa kuchukua maelekezo yaliyotolewa na Baraza la
Maaskofu Katoliki Tanzania.
Pia kujikinga kwa kufuata maelekezo ya
serikali na wataalamu wa afya.
Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki Mwanza
Askofu Mkuu Renatus Nkwande amewataka waamini wake (Mwanza na Bunda) kuendelea
kuchukua tahadhari hasa kwa wale wanaoishi bvijijini kwamba wavae barakoa na
kunawa mikono kila wakati.
“Seikali yetu na wataalamu wa afya
wameshasema hakuna dawa ya ugonjwa huu hivyo ninawasisitiza wajitahidi kufuata
maelekezo ya serikali.
Pia Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania
limetoa maelekezo mbalimbali ya kujikinga kwenye ibada ,mbalimbali hayo
yazingatiwe maana ugonjwa huu kweli upo,” amesema.

Ukiwa umefanya kazi maisha yako yote kujenga familia na urithi, huwezi kuruhusu kivuli cha mtu wa tatu kiiharibu katika miezi michache tu. Niligundua kuwa mabadiliko ya ghafla ya tabia ya mume wangu yalikuwa kuingiliwa kiroho, si tu mgogoro wa katikati ya maisha.
ReplyDeleteNiliwasiliana na Mystic Kakaa kwa ajili ya uingiliaji kati wa kibinafsi. Kazi yake ilikuwa ya upasuaji. Alitambua kivuli na kukiondoa kabisa bila drama yoyote ya umma. Ndani ya siku 5, umakini wa mume wangu ulirudi nyumbani kwetu na katika mustakabali wetu. Ikiwa unalinda maisha yenye thamani kubwa na unahitaji bwana anayeelewa busara, wasiliana naye kwa: dawnacuna314@gmail.com
WhatsApp: +2349046229159
Yeye ndiye kiwango cha dhahabu.
Kwa uchawi wa upatanisho wa uhusiano/ndoa.
Uchawi wa kumfanya mpenzi wako wa zamani/mwenzi wako aombe msamaha.
Uchawi wa kumrudisha mpenzi wako/kumvutia mpenzi mpya.
Uchawi wa kurejesha mali/pesa zilizoibiwa.
Mabadiliko ya umbo/Uchawi wa kutoweka.
Uchawi wa kushinda bahati nasibu/kesi ya mahakama. Na zaidi
I want to give a testimony on how I got cured from Herpes Virus. Few months back I was having some symptoms. I went to see a doctor and many blood tests were done on me, later on I was told I had Herpes. My doctor told me that there’s no cure for Herpes. I felt bad, I went online searching for a possible cure for Herpes Virus, I saw a post of Dr. Dawn, a herbal doctor that’s helping people get cured from Herpes.Cancer.HIV and more I contacted him and told him how I’m feeling. He said his herbal medicine can cure me. He sent me the medicine via UPS delivery service and I received the medicine 6 days after he sent it, i took the medicine as prescribed by him. Before I completed the medication the symptoms stopped. I went to the doctor and carried out another blood test, surprisingly I was Negative. I haven’t had any symptoms anymore. Dr. Dawn is great and you can
ReplyDeletecontact on WhatsApp: +2349046229159
Gmail ( dawnacuna314@gmail.com )
If you need herbal medicine to cure any chronic or sexual transmitted disease's like.
HERPES.
CANCER.
HIV/AID'S and more