Prof Makubi: Corona bado ipo wananchi msibweteke

MGanga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi amewataka  wananchi waendelee kuchukua tahadhari  juu ya maambukizi ya ugonjwa wa covi 19 unaosababishwa na virusi vya corona.
Prof. Makubi ameeleza hayo  hivi karibuni alipokuwa anazungumza na  Gazeti Kiongozi kuhusu kile kinachosadikiwa na jamii kuwa tayari kuna dawa ya corona.
“Ninachiotaka kuwaambia wananchi ni kwamba, hakuna dawa ya corona. Mpaka sasa dawa haijapatikana nna ile tuliyoleta kutoka Madagascar bado inafanyiwa uchunguzi kujiridhisha.
Wananchi hawa vijana na wale waishio vijijini wanapaswa waelewe kuwa,  virusi vya corona havibagui umri wala mahali.
Vijijini corona ipo tena ni rahisi kusambaa hasa kwenye minada na magulio. Hivyo waendelee kuchukua tahadhari kama zinavyoelekezwa  na serikali pamoja na wataalamu wa afya  ikiwemo WHO.
Amewataka wenyeviti wa Mitaa, Vijiji, kata nk. kuweka mikakati ambayo itawasababisha wananchi  waendelee na shughuli zao za kiuchumi. 
“Kwa mfano minada inaweza kuongezwa kwenye maeneo ambayo yako wazi. Mnada wa wawanyama peke yake, wa vyakula peke yake, wa nguo nk.
Na kila anayeingia avae barakoa. Kwa watu wa kijijini wanaweza kujitengenezea barakoa kwa kutumia vitambaa vya cotoni vyenye leya mbili, wawe na maji na sabuni ya kunawa mikono na kuepuka kugusana. Wakae umbali unaopendekezwa na wataalamu,” amesema.
Amewataka wananchi waepuke mikusanyiko isiyo na maana na kama hakuna lazima ya kwenda kwenye mikusanyiko wananchi watulie majumbani mwao.
“Ninawashukuru wananchi kwa kuonesha juhudi ya namna ya kujikinga wengi wanavaa barakoa, wananawa mikono hivyo waendelee hivyo hivyo maana hakuna dawa.
Kwenye baa  waweke maji, wahudumu wanawe, wateja wanawe
Meza ziwe mbalimbali viti kadhalika,” amesema.
Amewataka wananchi kupuuza taarifa za uongo zinazoenea mtaani kuwa kuna dawa ama kuwa ugonjwa huu hauui, na kwamba vijijini wapo salama.
Ugonjwa huu upo na mpokee taarifa  na maelekezo  kutoka kwa serikali, wizara ya afya na wataalamu wa afya tu. Msisikilize porojo za mtaani,” amesisitiza.

Kwa upande wake Askofu wa Jimbo Katoliki Rulenge Ngara Mhashamu Severine-Niwemugizi amewasisitiza waamini wa jimbo hilo kufuata malekezo wanayopewa na serikali pamoja na wataalamu wa afya na wasipuuzie kwasababu wapo waamini  wanaotunga maelekezo ya ugonjwa huo.
“Nina wasiwasi juu ya wananchi wanaoishi vijijini kwani ugonjwa huu ukiingia kijijini kwa kasi wananchi wanafariki sana kwani katika shughuli zangu za kichungaji nikipita mtaani ninaona vijiweni wananchi hawana ile social distance(umbali kati ya mtu na mtu.
Wengine ukiwaambia kunawa mikono wanaona ni matumizi mabaya  ya maji kwani kwao maji ni kama mali ghafi kwasababu ya ukosefu wa maji vijijini.
Amesema elimu vijijini bado inahitajika kwa wananchi wa vijijini ambao wanauchukulia ugonjwa huu kwamba si wao,” amesema.
Akieleza kufungua shughuli za ibada kupitia barua yake ya kichungaji aliyoitoa hivi karibuni amewataka waamni wake kuendelea na shughuli za ibada kwa kuchukua maelekezo yaliyotolewa na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania.
Pia kujikinga kwa kufuata maelekezo ya serikali na wataalamu wa afya.
Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki Mwanza Askofu Mkuu Renatus Nkwande amewataka waamini wake (Mwanza na Bunda) kuendelea kuchukua tahadhari hasa kwa wale wanaoishi bvijijini kwamba wavae barakoa na kunawa mikono kila wakati.
“Seikali yetu na wataalamu wa afya wameshasema hakuna dawa ya ugonjwa huu hivyo ninawasisitiza wajitahidi kufuata maelekezo ya serikali.
Pia Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania limetoa maelekezo mbalimbali ya kujikinga kwenye ibada ,mbalimbali hayo yazingatiwe maana ugonjwa huu kweli upo,” amesema.


Comments

Popular posts from this blog

SALA YA ASUBUHI:SALI HIVI..

Ujio wa Wamisionari wa Kwanza Tanzania Bara (2)

HISTORIA YA SHEREHE YA MOYO MTAKATIFU WA YESU