Posts

Maaskofu Katoliki Tanzania wapewa mafunzo juu ya Uongozi Bora

Image
Na Sarah Pelaji, Dar es Salaam B araza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) kwa ushirikiano na Umoja wa Mabaraza ya Maaskofu Afrika Mashariki AMECEA na Missio, wametoa mafunzo kwa Maaskofu wa Kanisa Katoliki juu ya uongozi Bora. Mafunzo hayo    ya siku tano yamefanyika kuanzia Januari   14-19, mwaka huu   katika Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania Kurasini jijini   Dar es Salaam. Maaskofu hao wanajengewa uwezo juu ya Uongozi na   Usimamizi wa taasisi, Uongozi Endelevu; Umoja wa Kanisa Katoliki pamoja na Ushauri na Usimamizi. Awali Katibu Mkuu wa AMECEA Padri Anthony Makunde ameeleza kuwa, mafunzo hayo ni ya awamu ya pili   ambapo awamu ya kwanza yalikuwa yanafadhiliwa na Baraza la Maaskofu Katoliki Marekani sasa awamu ya pili yanafadhiliwa na Baraza la Maaskofu Katoliki Ujerumani kupitia shirika lao la Missio. Aidha ameeleza kuwa alifanya safari   na Rais wa AMECEA Mhashamu Charles Kasonde kwenda kukutana na Rais wa Missio Aach...

Mamia wamzika Padri Mwechibindu

Image
Na. Philipo Josephat - Dsm M amia ya waamini kutoka Parokia mbalimbali za Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, mapadri, watawa na maaskofu kutoka majimbo mbalimbali nchini na viongozi mbalimbali wa serikali   wamejitokeza kumzika marehemu Padri Andrew Mwachibindu aliyefariki katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili usiku wa January 12, 2019. Akiongoza Ibada ya Misa Takatifu ya kumwombea marehemu kabla ya mazishi yake yaliyofanyika katika Kituo cha wafia dini Pugu Askofu Mkuu Mwandamizi wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam Mhashamu Yuda Thadei Ruwaichi amemtaja marehemu kama mtu aliyekuwa mtulivu, mwenye nidhamu na mipango chanya ya utumishi. Aliyeongozwa na uchaji wa kimungu na mchungaji msikivu aliyependa kufanya yote vema. Amesema katika maisha mwanadamu anapitia magumu na mateso mazito na anapokabiliwa na mateso hayo huwa anakuwa na hofu hivyo kila mwanadamu anapaswa aongozwe kwa imani yake kwa Kristo anapokabiliwa na kifo. Ameongeza kuwa wakristo wote hawanabudi...

Baraza la Makanisa Ulimwenguni lalaani mauaji Kenya

Image
Kenya D r. Olav Fykse Tveit, Katibu mkuu wa Baraza la Makanisa Ulimwenguni katika taarifa yake kwa vyombo vya habari anasema, wamesikitishwa sana na shambulizi la kigaidi lililotokea katika hoteli ya DusitD2 eneo la 14 Riverside Drive, Jijini Nairobi siku ya Jumanne, tarehe 15 Januari 2019 na kusababisha watu zaidi ya 15 kupoteza maisha na wengine wengi kujeruhiwa. Baraza la Makanisa Ulimwenguni linapenda kutuma salam za rambi rambi kwa wale wote walioguswa na maafa haya na kwamba, linaziombea roho za marehemu zipate pumziko la milele huko mbinguni! Kwa majeruhi waweze kupona haraka na hatimaye, kurejea katika shughuli zao za kila siku! Baraza la Makanisa Ulimwenguni, kwa mara nyingine tena, linachukua fursa hii kulaani vikali vitendo vyote vya kigaidi vinavyohatarisha usalama wa raia na mali zao. Waamini na watu wote wenye mapenzi mema, hawana budi kujitokeza si tu kulaani vitendo hivi vya kigaidi, bali kuunga mkono mchakato wa kukuza na kudumisha misingi y...