Posts

Askofu Chengula: Padri bora hanywi pombe kilabuni

Image
Na Izack Mwacha, Mbeya WITO umetolewa kwa viongozi wote wa kiroho hususani mapadri kutambua kuwa kunywa pombe kilabuni siyo tabia za padri mzuri ambaye anamuwakilisha Kristo Duniani. Wito huo umetolewa na Askofu wa Jimbo Katoliki Mbeya Mhashamu Evaristo Chengula wakati wa Ibada ya Misa Takatifu ya Daraja ya upadri kwa Shemasi Jacob Machibya, iliyofanyika Parokia ya Chunya Jimboni Humo. Katika homilia yake Askofu Chengula amebainisha kuwa yapo mambo mengi ambayo yanawezesha kujua kiongozi bora na muadilifu mbele za watu, lakini kipimo ambacho pia kitaimarisha zaidi   nafasi ya kiongozi kama padri muwakilishi wa Kristo ni pamoja na kufanya mambo sahihi na kwa wakati. “Sidhani kama litakuwa jambo la busara kwa padri kukaa kilabuni na kuanza kunywa pombe, hapana hiyo siyo tabia njema” amesisitiza Askofu chengula. Katika hatua nyingine Askofu Chengula amewaasa viongozi wa Halmashauri Walei kuwa na uwezo wa kuzungumza na mapadri wao bila ya kuwa na wasiwasi na jambo lolot...

TEC yawasilisha rai kwa serikali

Image
Yasisitiza kujenga jukwaa la majadiliano katika ukweli na uwazi  Na Sarah Pelaji, Dar es Salaam RAis John Pombe Magufuli wa Tanzania, Agosti 7, 2018 amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa Jumuiya ya Wakristo Tanzania, CCT pamoja na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania TEC, walioomba kukutana naye na kujitambulisha, Ikulu, Jijini Dar es Salaam. Ujumbe wa Jumuiya ya Wakristo Tanzania umeongozwa na Askofu Anikilisa Cheyo, Mwenyekiti na kwa upande wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, ujumbe umeongozwa na Askofu Gervas John Nyaisonga, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania. Kwa upande wake, Rais Magufuli amewahakikishia viongozi wa Makanisa kwamba, yuko pamoja nao na kuwataka kufanya kazi kwa kujiamini na kwa uhuru na ikiwa kama wanalo jambo lolote lile, wamjulishe na kwamba, atalishughulikia. Amewataka viongozi wa Makanisa kuwahubiria Watanzania amani, upendo na mshikamano pamoja na kuipenda nchi yao! Akizungumza na gazeti hili, Makamu...

Ufahamu juu ya tatizo la homa ya ini

Image
Na Josephat Wangwe TUNGALIKUA na mazoea ya kujali afya zetu na kujituma kwa moyo mkuu katika kuzitunza na kuziboresha kama tunavyotunza vitu vyetu vya thamani (Majumba, magari, simu, nk), basi gharama za matibabu tuzipatazo kila mwaka katika taifa letu zingepungua kwa kiasi kikubwa. Lakini kutokana na muitikio hafifu tulionao katika mambo yahusuyo afya basi tumejikuta tukilazimika kuishi na magonjwa mbalimbali ndani ya miili yetu, mengine yanaoneka waziwazi na mengine huwa yamejificha ndani ya miili yetu yakitumaliza kidogo kidogo. Homa ya ini (hepatitis) ni hali ya kuwepo kwa uvimbe (Inflammation) katika ini. Homa ya ini hutokana na sababu mbalimbali, Virusi vya homa ya ini ndio sababu kubwa kati ya sababu zinazopelekea kutokea kwa tatizo la homa ya ini. kuna aina tano (5) za ugonjwa wa homa ya ini zinazotambulika duniani yaani A,B,C,D na E ( Hepatitis A,B,C,D pamoja na E ). Utofauti huu unatokana na aina ya kirusi kilichomuingia mtu husika ( Hepatitis A virus-HAV, Hep...