Posts

Tabora kuenzi ndoto za Padri Nyamiti kuanzisha chuo cha muziki

Image
KUFUATIA kifo cha Padri Prof. Charles Nyamiti kilichotokea Mei 19, 2020 katika Hospitali ya Mt. Anna Ipuli, Jimbo Kuu Katoliki Tabora limedhamiria kuendeleza ndoto za mtaalamu huyo wa muziki hasa za kuanzisha chuo cha muziki. Akizungumza na KIONGOZI mapema wiki hii Mratibu wa Idara ya Liturujia, Jimbo Kuu Katoliki Tabora ambaye pia ni mwanafunzi wa muziki wa Padri Nyamiti, Padri Deogratius Mwageni, amesema kuwa Padri Nyamiti alikuwa anatamani kuanzisha chuo cha muziki na yeye mwenyewe alikubali kujitoa ili aweze kufudisha nadharia ya muziki na vitendo. “Kwa kuanzia alikuwa na wanafunzi watatu ambao ni waseminari walioko likizo na mpaka siku ya mwisho kabla ya kifo chake alikuwa anafundisha muziki. Siku hiyo ya Jumatatu alifundisha kwa muda mrefu tena bila kuchoka mpaka alipoombwa apumzike. Ndipo akaenda kupumzika kidogo na akiwa mapumzikoni hali yake ilibadilika hivyo akapelekwa hospitali na baada ya vipimo akakutwa ana malaria kali” ameeleza Padri Mwageni. Ameongeza kuwa alil...

Katibu Mkuu TEC: Wananchi msikebehi maelekezo ya serikali dhidi ya corona

Image
JAMII imetakiwa kutokuzikebehi na kuzibeza juhudi   zinazofanywa na serikali katika kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa hatari wa covid-19 unaosababishwa na virusi vya corona, badala yake itekeleze kwa vitendo maagizo na miongozo inayotolewa. Rai hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padri Charles Kitima katika mahojiano maalum na vyombo vya Habari nchini, yaliyofanyika katikati ya juma ofisini kwake Kurasini jijini Dar es Salaam. Amesema, Kanisa Katoliki nchini linaridhishwa na hatua zinazofanywa na serikali kupitia Wizara ya Afya katika mapambazo dhidi ya ugonjwa huu ulionea sehemu mbalimbali duniani, hivyo akasisitiza kwamba hakuna sababu ya baadhi ya watu ama makundi ya kijamii kuzibeza na kuzikebehi juhudi hizo. Katika kusisitiza zaidi amesema “Tuiache Serikali ifanye kazi yake kwa kutumia wataalam wa afya iliyonao na kila mmoja kwa nafasi yake, atoe ushirikiano kama inavyotakiwa…hili siyo tatizo la kukebehi wala kufanyia mzah...

Kumbukumbu ya miaka 15 tangu Mt. Papa Yohane Paulo II afariki dunia

Image
KAnisa Katoliki duniani Aprili 2 mwaka huu linakumbuka miaka 35 tangu Papa Yohane Paulo II (sasa Mtakatifu) afariki dunia. Mtakatifu Yohane Paulo II alifariki dunia tAprili   2 mwaka 2005, yaani miaka 15 iliyopita na kuacha ushuhuda wenye mvuto katika maisha ya binadamu. Kardinali Angelo Comastri, Mhudumu Mkuu wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatikani akitoa ushuhuda wa maisha ya Mtakatifu Yohane Paulo II, kama sehemu ya kumbukumbu ya miaka 15 tangu Mtakatifu Yohane Paulo II alipofariki dunia ameeleza kuwa; Hata leo hii, katika hofu, wasi wasi na taharuki ya kuenea kwa ugonjwa wa homa ya mapafu unaosababishwa na Virusi vya Corona, COVID-19, bado Kanisa linaamini kuwa Mtakatifu huyo   anaendelea kuiombea dunia na watu wa Mungu katika   dhoruba hii kali. Takwimu za maambukizi na vifo vinavyotokana na Virusi vya Corona inaonekana kuongezeka maradufu, kiasi cha kuwakatisha watu tamaa ya maisha. Watu wametikiswa kutoka katika undani wa maisha yao kiasi cha ...