KARDINALI PENGO APONGEZA JUHUDI ZA ASKOFU SANGU
n Na Joachim Mahona, Shinyanga. A SKOFU Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar-es-salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo amepongeza juhudi mbalimbali zinazofanywa na Askofu wa Jimbo Katoliki Shinyanga Mhashamu Liberatus Sangu za kulistawisha Jimbo na kutoa huduma mbalimbali za kijamii jimboni humo. Akizungumza mara baada ya kuongoza misa takatifu ya dominika ya kwanza ya majilio katika Kanisa Kuu la Mama Mwenye Huruma Ngokolo mjini Shinyanga wakati wa kuhitimisha ziara yake ya siku nne aliyoifanya jimboni Shinyanga, Kardinali Pengo amebainisha kuwa amepata faraja kubwa baada ya kutembelea miradi mbalimbali na kuona jinsi Askofu Sangu anavyofanya juhudi kubwa za kulistawisha Jimbo kwa kushirikiana na mapadri na waamini kwa kipindi kifupi tu cha miaka miwili tangu aanze utume wake. “Narudi Dar-es-Salaam nikiwa naamini kuwa Jimbo hili limepiga hatua kubwa katika hali ya kushangaza, nilikuwa na wasiwasi wakati wa kumwekea mikono siku ile tuliyokuwa tukimweka wakfu kuwa Askofu wa Shin...