Askofu Dallu akemea uchumba sugu
Na Sr. Tuzo Nyoni OSB, Songea WAamini wameaswa kuachana na tabia ya kuishi uchumba sugu bila kufunga ndoa. Badala yake wafunge ndoa ili wapate kupokea sakramenti mbalimbali katika kanisa. Hayo yamesemwa hivi karibuni na Askofu Mkuu Damian Dallu wa jimbo Kuu Katoliki Songea, wakati akihubiri katika Misa Takatifu ya jubilee ya miaka hamsini ya Parokia ya Mtakatifu Martin wa Tur Mpandangindo iliyopo katika jimbo Kuu Katoliki Songea. Askofu Dallu amesema kuwa, suala la uchumba sugu limekuwa likijitokeza katika parokia nyingi jimboni Songea na kuhimiza kuwa, waamini hawana budi kushika amri za Mungu na Kanisa kikamilifu. Ameongeza kuwa, suala la kutoa zaka kwa waamini ni la msingi na kwamba waamini waachane na tabia ya kutoa zaka kwa Kanisa wakati wanapokuwa na majukumu ya kusimamia na kupokea sakramenti tu. Akizungumzia sherehe ya Jubilei ya miaka 50 ya parokia hiyo ya Mpandangindo Askofu Dallu amesema , anatoa shukrani kwa uwepo wa wamisionari Wabene...