Jamii yatakiwa kuthamini wazee
Jimmy Mahundi, Mtwara Jamii imetakiwa kuacha tabia ya kuwatelekeza wazee na kuwaacha waishi katika mazingira magumu. Kauli hiyo imetolewa na wazee walioshiriki kongamano la wazee katika kuadhimisha siku ya wazee duniani ambapo kitaifa imefanyika mkoani Mtwara na kuhudhuliwa na wawakilishi wa wazee kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini. Wazee hao wamedai kuwa kwa sasa wengi wao wanaishi maisha magumu sana kutokana na vijana wao waliowasomesha kwa shida na taabu leo wanawaona mizigo na wanashindwa kuwasaidia. “Baadhi ya watoto wetu wanatuona kama mizigo maana hatuna nguvu tunawategemea kwa kila kitu. Pia wanasahau kutimiza wajibu wao wa kulea wazazi wao kama sisi tulivyotimiza wajibu wetu kuwalea na kuwasomesha. Hivyo wanaposahau kuwa nasi pia tuliwalea na kuwapa elimu, wanajiona kuwa mafanikio wanayopata ni kutokana na juhudi zao tu. Inasikitisha kuona wazee wanaishi maisha magumu sana kwa kuwa watoto wao wanawaona kuwa ni mizigo isiyobebeka”amesema Mzee...