Posts

Kamati ya Umoja wa Dini mbalimbali nchini (CCT, TEC na BAKWATA) imeandaa mafunzo kwa wanawake juu ya 'Wanawake na uongozi wa kuchaguliwa' unaofanyika katika Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania kuanzia Sepemba 4 hadi 5 mwaka 2019.

Image
Image
Askofu Mkuu Protas Rugambwa akitoa Daraja Takatifu la Upadri kwa mashemasi wawili jimboni Kigoma (Na Mpiga picha wetu). Mapadri wapya wa Jimbo Katoliki Kigoma wakitoa baraka kwa Askofu Joseph Mlola ALCP/OSS (Wa kwanza waliopiga Magoti) na Askofu Mkuu Protas Rugambwa  baada ya kupata Daraja Takatifu la Upadri hivi Karibuni (Na Mpiga Picha wetu).

DC Songwe apongeza utendaji wa Askofu Nyaisonga

Image
Na Thompson Mpanji, Songwe MKUU wa Wilaya   ya Songwe,Samwel Jeremiah   amemuelezea Askofu Mkuu   wa Jimbo Kuu Katoliki la Mbeya,Mhashamu Gervas Nyaisonga   kuwa ni mtu wa aina yake ambaye   amejawa hekima na busara katika uchungaji wake. Mkuu huyo wa Wilaya amesema hayo   alipokuwa mgeni rasmi   katika mahafali   ya tisa ya kuwaaga   wahitimu   wa mafunzo   ya Uuguzi na Ukunga   katika ngazi ya stashahada katika Chuo cha Mwambani, kilichopo Kata ya Mkwajuni, wilaya ya Songwe, mkoani Songwe.   “Kwa kweli nimemshangaa   na kumuona ni kiongozi wa ajabu na nilikuwa nikimsikia na leo nimejionea nilipoambiwa kuwa yeye Askofu Mkuu   amekataa kuwa mgeni rasmi na kupendekeza lazima awe Kiongozi wa Serikali... Nilijiuliza sana kwamba kwanini Baba Askofu amefanya hivyo...nikasema Baba amejawa na unyenyekevu, hekima na busara   za pekee,”anasema Mkuu wa wilaya hiyo na kuongeza; “Niseme tu Baba Askofu ...

Kardinali Pengo afanya ziara ya kichungaji Shinyanga

Image
N a Natoly Salawa ±Shinyanga ASkofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo amewataka mapadri kuambatana daima na Kristo katika utume wao badala ya kujiambatanisha na malimwengu. Kadinali Pengo ameyabainisha hayo katika Kanisa Kuu Mama Mwenyehuruma Ngokolo Shinyanga wakati wa mahubiri yake katika adhimisho la Ekaristi Takatifu na utowaji wa Daraja Takatifu la Upadri kwa mashemasi sita katika sherehe ya Kupalizwa Mbinguni Bikira Maria iliyofanyika 15 Agosti, 2019. Katika ujumbe wake,Kadinali Pengo amewataka mapadri hao wapya kwenda kufanya utume wao kwa uaminifu huku wakitambua kuwa upadri ni   kujitoa sadaka kwa Mungu, hivyo wasifanye   utume wao kinyume na matarajio ya Wakristo ambao wanamategemeo makubwa juu yao na badala yake wamtangulize Kristo   katika huduma yao kwa Kristo na Kanisa lake. Aidha Kadinali Pengo ametoa wito kwa   waamini wa jimbo Katoliki Shinyanga kuendelea kuwaombea mapadri wapya na mapa...