Posts

Askofu Ruzoka awafunda waseminari waliohitimu Falsafa Kipalapala

Image
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Tabora Mashamu Paul Ruzoka amwewaasa Mafrateri wa seminari Kuu Ya Mtakatifu Paulo Mtume Kipalapala kuwa waaminifu kwa Neno la Kristo na kumfuata Kristo kwa kuishi maisha ya ufukara na kukaa mbali na mali za dunia. Rai hiyo ameitoa hivi karibuni katika Kanisa la seminari hiyo alipokuwa akitoa mahubiri yake yaliyolenga kumshukuru Mungu kwa neema nyingi alizowajalia mafrateri wa mwaka wa nne waliohitimu malezi yao seminarini hapo. Akizungumza wakati wa Misa Takatifu Askofu Mkuu Ruzoka amewahimiza mafrateri hao wanaoenda kufanya utume wao katika sehemu mbalimbali za majimbo ya Tanzania kuishi yale walioyapata wakati wa malezi yao . “ Nendeni mkatoe harufu nzuri ili kwa wale mtakaowahudumia wamuone Kristo kupitia nyie”, Askofu Ruzoka amesema. Aidha katika mahubiri yake Askofu Ruzoka amewaomba mafrateri wahitimu kujua sasa wameongezeka kimo na ufahamu hivyo hawanabudi kutumia elimu na maarifa waliyoyapata kwa faida ya Kanisa na wanapaswa kuhakikish...

Ask. Minde: Watoto wanaopelekwa seminari waandaliwe kiroho

Image
Askofu wa Jimbo Katoliki Kahama Mhashamu Ludovick Minde ALCO/OSS ametoa wito kwa wazazi na walezi kuwa   wanapaswa kuwaandaa kiroho na malezi ya wito watoto wanaowapeleka kujiunga na seminari. Wito huo ameutoa wakati wa Misa Takatifu ya Sherehe ya Seminari ndogo ya Malkia wa Mitume, Ushirombo   iliyoambatana na ufunguzi wa Bwalo la kulia chakula la seminari hiyo. Askofu Minde amesema katika mambo ya Mungu yanapaswa kuongozwa na Roho Mtakatifu kuanzia kwenye familia. Familia zidumu katika maisha ya uongofu, sala na kuwaandaa watoto kwa miitombalimbali ukiwemo wito wa upadri hata kabla hawajajiunga na seminari. “Tusifanye mambo peke yetu tumuombe   Mungu atuongoze katika maisha na mipango yetu kwa kufaata mafundisho ya Kanisa.   “Tunapoandaa   mambo yetu tusiongozwe   na jazba hatuwezi kuwa na mafanikio mazuri kwenye maisha yetu kama hatumshirikishi Mungu,” amesema Askofu Minde. Amewataka waamini   kuomba hekima   ya Mungu kwa moyo w...

Papa Francisko alitaka Kanisa kulinda na kutetea uhai

Image
Baba Mtakatifu Francisko, Jumatano tarehe 12 Juni 2019 kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican, baada ya Katekesi kuhusu Safari ya Injili Ulimwenguni mintarafu Kitabu cha Matendo ya Mitume, amewaambia waamini na mahujaji waliofurika kwa wingi mjini Vatican kwamba, Kanisa limezaliwa kutoka katika nguvu ya Fumbo la Ufufuko. Mwanga wa Kristo Mfufuka katika Jumuiya ya kwanza ya Wafuasi wa Kristo umevunjilia mbali ubinafsi na woga dhidi ya wafuasi wengine. Mwanga huu ukawahamasisha kuwa ni vyombo na mashuhuda wa ujenzi wa Kanisa hadi miisho ya dunia! Huko, wakatangaza na kushuhudia upendo wa Mungu uliomwilishwa katika umoja na ushirikiano; ushuhuda na udugu! Hii ni changamoto kwa Wakristo kuendelea kuishi katika umoja unaofumbatwa katika utofauti wao kama ulivyoshuhudiwa na Kristo Yesu. Baba Mtakatifu anaendelea kuwakumbusha waamini kwamba, maisha ni zawadi kubwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Kama waamini wanaitwa na kuhamasishwa kulinda, kuitunza na kuidumisha, tang...