Posts

Balozi wa Baba Mtakatifu afanya ziara ya kichungaji Jimboni Musoma

Image
Na Veronica Modest- Musoma B alozi wa Baba Mtakatifu nchini Askofu Mkuu Marek Solczynski   amefanya ziara ya kichungaji kwa mara ya kwanza tangu kuteuliwa kwake,katika Jimbo   Katoliki   Musoma kuan zia Oktoba   02 hadi 09   mwaka huu. Katika ziara hiyo Balozi huyo ametembelea maeneo mbalimbali ambapo Oktoba 02 alikuwa katika Parokia ya Kiabakari na aliongoza Ibada ya uzinduzi wa kituo cha Hija ya Huruma ya Mungu Kiabakari na kukipandisha kutoka hadhi ya Kijimbo hadi hadhi ya Kitaifa pamoja na kubariki Kikanisa (chapel)   cha Bikra Maria. Ametembelea kliniki ya meno na macho katika kituo cha afya cha Blessed Pier Giorgio Frassati Kiabakari na kubariki wagonjwa. Akiwa Parokiani hapo alikutakutana pia na mapadri ,watawa na waamini wa udekano wa Butiama. Oktoba 03 Balozi huyo   akiwa katika Kanisa Kuu la Musoma alishiriki kusali Rozari Takatifu na waamini wa parokia hiyo na aliongoza   ibada ya Baraka Kuu na baadae alikutana na ...

Serikali yapokea ripoti ya utafiti wa viongozi wa dini kuhusu afya

Image
Sarah Pelaji na Rodrick Minja, Dodoma S erikali yapokea ripoti ya Viongozi wa dini kuhusu hifadhi ya jamii kwenye sekta ya afya Octoba 4 mwaka huu katika Mkutano wa Viongozi wa dini mbalimbali uliofanyika katika Ukumbi wa Mt. Gaspari Dodoma. Akipokea Ripoti hiyo kwa niaba ya serikali Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii Dokta John Jingu amebainisha kuwa jukumu kubwa la serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dokta John Pombe Magufuli ni kuhakikisha kuwa msisitizo mkubwa ni kuwahudumia walio wanyonge. Amesema kuwa viongozi wa dini wamekuwa wakihubiria waamini wao juu ya huduma kwa wanyonge na maskini zaidi pamoja na kuwasaidia walio wadogo. “Serikali yetu tangu ipate uhuru imekuwa ikisisitiza hivyo wakati iliposisitiza kupiga vita maadui watatu ambao ni ujinga, maradhi na umaskini ilikuwa inamaanisha hivyo” aliongeza Dokta Jingu. Hata hivyo amesema kauli ya Rais Magufuli ya kuwa yeye ni Rais wa wanyonge i...