Posts

Matukio katika Misa Takatifu ya kilele cha Kongamano la Ekaristi Takatifu Jimbo Katoliki Morogoro

Image

Napata nakala yako ya gazeti la Kiongozi wiki hii

Image

Matukio mbalimbali yaliyojiri katika Adhimisho la Misa Takatifu ya kumpokea Askofu Mkuu Mwandamizi wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es salaam Mhashamu Yuda Thadei Ruwaich, lililofanyika katika Kanisa Kuu la Mt. Yosefu Septemba 7, 2018.

Image

Hii ndiyo nguvu ya Kanisa Katoliki Tz

Image
Na Na Pascal Mwanache, Dar es salaam L ikiwa linaadhimisha Jubilei ya Miaka 150 ya Uinjilishaji Tanzania Bara, Kanisa Katoliki nchini limeendelea kuwa kielelezo katika utoaji wa huduma za elimu, afya na za kijamii bila upendeleo hasa kwa watanzania wanaoishi maeneo ya vijijini. Akifungua Mkutano Mkuu wa Idara ya Afya ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Askofu wa Jimbo Katoliki Bunda Mhashamu Renatus   Nkwande amesema kuwa Kanisa litaendelea kutoa huduma za afya na elimu nchini kwa kufuata yale yaliyofanywa na Kristo, ambaye alitibu na kufundisha. “Endeleeni kushiriki kikamilifu, shirikishaneni mang’amuzi yenu katika utoaji huduma ili kuwafanya wale tunaowahudumia waone kuwa ufalme wa Mungu umetamalaki” ameeleza Askofu Nkwande ambaye pia ni Mwenyekiti wa Idara ya Afya TEC. Aidha Askofu Nkwande ametoa rai kwa wajumbe wa mkutano huo kujikita katika kufanya utafiti, uvumbuzi na mafunzo badala ya kujikita katika kutibu peke yake. Kwa upande wake Katibu Mkuu ...

Fanyeni maamuzi sahihi juu ya imani yenu-Ask. Mdoe

Image
Na Jimmy mahundi, Mtwara WA AAMINI wa Jimbo Katoliki Mtwara wametakiwa kufanya maamuzi sahihi katika masuala ya kiimani na kuacha kutangatanga pasipo kufanya uchambuzi wa kina. Hayo yamesemwa hivi karibuni na Askofu wa Jimbo Katoliki Mtwara Mhashamu Titus Mdoe wakati wa Ibada ya Misa Takatifu iliyoenda sambamba na utoaji wa Sakramenti ya Kipaimara katika Kanisa la Mtakatifu Paulo Parokia ya Majengo. Askofu Mdoe amesema hayo kufuatia uwepo wa waamini wengi wanaohangaika na kuchukua maamuzi katika mambo yanayohusu imani pasipo kufanya uchambuzi na kubaini ukweli. “Kabla ya kufanya maamuzi fanyeni uchambuzi na kubaini baya na zuri, kisha baya liache” amesema Askofu Mdoe. Aidha amebainisha kuwa wapo watu wengi katika nyakati hizi wanaotangatanga katika imani na kuwataka kuachana na kuhangaika bali wawe na misimamo ya kweli katika imani yao hiyo. Pia katika nafasi hiyo, amewakumbusha wazazi na walezi kuwafundisha watoto wao kuchagua na kufanya maamuzi sahihi kwa kuwa huo ni ...