Maaskofu wa Chile wakutana na Papa mkutano wa dharura
Roma M AASKOFU wa Chile wapo Roma wiki hii kwa ajili ya mkutano wa dharura na Papa Fransisko, ambaye anataka kukabiliana na mgogoro wa unyanyasaji wa kijinsia uliojificha katika Kanisa nchini mwao. Maaskofu thelathini na moja wa Chile watashiriki, pamoja na wachache waliostaafu. Mkutano huo utaanza Mei 15-17 ambapo Kardinali Cardinal Francisco Javier Errázuriz wa Chile anahusika zaidi na mzozo huo kwani anashutumiwa na waathirika wa unyanyasaji na Mahakama ya Jinai ya Vatikani kufunika kesi ya Padri Fernando Karadima, ambaye alikuwa kuhani maarufu nchini Chile, baada ya kupata hatia ya unyanyasaji wa kijinsia miaka kadhaa iliyopita. Taarifa kutoka Vatikani zimeeleza kuwa, mkutano utafanyika kwa siri, na kwamba Baba Mtakatifu angewasilisha maaskofu wa Chile kwa hitimisho lake kwa misingi ya hati ya 2300 ya uchunguzi wake maalum. Maaskofu wa Chile wanasema kuwa, makosa yalifanyika wakati wa kushughulikia kesi za unyanyasaji wa kijinsia wa...