‘Haki itendeke kwa wote’ Na Pascal Mwanache, Morogoro NCHI inapojiandaa kutekeleza haki ya msingi ya kidemokrasia ya raia wote kuchagua viongozi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji hapo 2019 wito umetolewa kwa vyombo husika kuwa walinzi wa watanzania wote kwa haki bila kuminya haki za watu wengine. Wito huo umetolewa na Askofu wa Jimbo Katoliki Morogoro Mhashamu Telesphor Mkude katika Misa Takatifu ya Jumatano ya Majivu iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Mt. Patriki Morogoro. Askofu Mkude amesema kuwa kila mmoja anapaswa kujitathmini iwapo amekuwa mlinzi wa mwingine au amewatendea mema wale tu waliokuwa upande wake. “Tunapojiandaa na uchaguzi mdogo katika serikali za mitaa tujiulize, mtazamo wetu juu ya jirani upoje? Tumekuwa walinzi kweli. Tumekuwa walinzi wa watanzania wote? au tunakwenda na mawazo gani, kwamba ndugu kwangu mimi ni yule ninayetoka naye mtaa mmoja, au familia moja tu? Mwingine siyo ndugu yangu? Kama mkiwapenda wale wanaowapenda t...